Zaburi 12
12
Zaburi 12
Kuomba msaada
Kwa mwimbishaji. Mtindo wa sheminithi. Zaburi ya Daudi.
1 Bwana tusaidie, kwa kuwa wacha Mungu wametoweka;
waaminifu wametoweka miongoni mwa wanadamu.
2Kila mmoja humwambia jirani yake uongo;
midomo yao ya hila huzungumza kwa udanganyifu.
3 Bwana na akatilie mbali midomo yote ya hila
na kila ulimi uliojaa majivuno,
4ule unaosema, “Kwa ndimi zetu tutashinda;
midomo ni mali yetu, bwana wetu ni nani?”
5“Kwa sababu wanyonge wanaonewa,
na wahitaji wanalia kwa uchungu,
nitainuka sasa,” asema Bwana.
“Nitawalinda kutokana na wale
wenye nia mbaya juu yao.”
6Maneno ya Bwana ni safi,
kama fedha iliyosafishwa katika tanuru,
iliyosafishwa mara saba.
7Ee Bwana, utatuweka salama
na kutulinda na kizazi hiki milele.
8Watu waovu huenda wakiringa kila mahali
wakati yule aliye mbaya sana
ndiye anayeheshimiwa miongoni mwa watu.
Iliyochaguliwa sasa
Zaburi 12: NENO
Kuonyesha
Shirikisha
Nakili

Je, ungependa vivutio vyako vihifadhiwe kwenye vifaa vyako vyote? Jisajili au ingia
Neno: Biblia Takatifu™ Neno™
Hakimiliki © 1984, 1989, 2009, 2015, 2025 na Biblica, Inc.
Imetumiwa kwa ruhusa. Haki zote zimehifadhiwa duniani kote.
Kiswahili Contemporary Version™
Copyright © 1984, 1989, 2009, 2015, 2025 by Biblica, Inc.
Used with permission. All rights reserved worldwide.