Chapa ya Youversion
Ikoni ya Utafutaji

Hesabu 23:18-24

Hesabu 23:18-24 NEN

Ndipo Balaamu akasema ujumbe wake: “Balaki, inuka na usikilize, nisikie mimi, wewe mwana wa Sipori. Mungu si mtu, hata aseme uongo, wala yeye si mwanadamu, hata ajute. Je, anasema, kisha asitende? Je, anaahidi, asitimize? Nimepokea agizo kubariki; amebariki, nami siwezi kubadilisha. “Haijaonekana bahati mbaya katika Yakobo, wala taabu katika Israeli. BWANA, Mungu wao yu pamoja nao, nayo sauti kuu ya Mfalme imo katikati yao. Mungu aliwatoa kutoka Misri; wao wana nguvu za nyati. Hakuna uchawi dhidi ya Yakobo, wala hakuna uaguzi dhidi ya Israeli. Sasa itasemwa kuhusu Yakobo na Israeli, ‘Tazama yale Mungu aliyotenda!’ Taifa lainuka kama simba jike; linajiinua kama simba ambaye hatulii mpaka amalize kurarua mawindo yake na kunywa damu ya mawindo yake.”

YouVersion hutumia vidakuzi kubinafsisha matumizi yako. Kwa kutumia tovuti yetu, unakubali matumizi yetu ya vidakuzi kama ilivyoelezwa katika Sera yetu ya Faragha