Chapa ya Youversion
Ikoni ya Utafutaji

Nehemia Utangulizi

Utangulizi
Vitabu vya Ezra na Nehemia vinakwenda sambamba na vitabu vya Mambo ya Nyakati, vikisimulia habari zinazofuata matukio ya Mambo ya Nyakati. Kitabu cha Nehemia kimepewa jina la mhusika wake mkuu ambaye ni Nehemia. Katika andiko la Kiebrania, kitabu hiki ni sehemu ya kitabu cha Ezra. Kuna uwezekano mkubwa sana kwamba katika kipindi hiki nabii Malaki alikuwa akihudumu.
Mwandishi
Kuna uwezekano mkubwa kwamba Nehemia au Ezra, au wote wawili ndio walioandika kitabu hiki, kwani mwanzoni Ezra na Nehemia vilikuwa kitabu kimoja.
Kusudi
Habari za kurudi kwa Wayahudi kutoka uhamishoni, na kujengwa kwa ukuta wa Yerusalemu.
Mahali
Yerusalemu.
Tarehe
Kuna uwezekano hiki kitabu kiliandikwa miaka ya 445–432 K.K.
Wahusika Wakuu
Nehemia, Ezra, Tobia na Sanbalati.
Wazo Kuu
Kitabu hiki kinaonyesha kutimizwa kwa unabii wa Zekaria na Danieli kuhusu kujengwa upya kuta za Yerusalemu.
Mambo Muhimu
Kujengwa kwa ukuta wa Yerusalemu, na kurejezwa kwa utaratibu wa ibada.
Mgawanyo
Nehemia anazijenga kuta (1:1–7:3)
Mabadiliko chini ya Ezra (7:4–10:39)
Mipango ya Nehemia (11:1–13:31).

Iliyochaguliwa sasa

Nehemia Utangulizi: NEN

Kuonyesha

Shirikisha

Nakili

None

Je, ungependa vivutio vyako vihifadhiwe kwenye vifaa vyako vyote? Jisajili au ingia

YouVersion hutumia vidakuzi kubinafsisha matumizi yako. Kwa kutumia tovuti yetu, unakubali matumizi yetu ya vidakuzi kama ilivyoelezwa katika Sera yetu ya Faragha