Chapa ya Youversion
Ikoni ya Utafutaji

Marko 2:1-5

Marko 2:1-5 NENO

Baada ya siku kadhaa Yesu alirudi Kapernaumu, watu wakasikia kwamba yupo nyumbani. Watu wengi wakakusanyika, kiasi kwamba hapakubaki nafasi yoyote hata mlangoni! Naye akawahubiria Neno. Ndipo baadhi ya watu wakaja wakamletea Yesu mtu aliyepooza, akiwa amebebwa na watu wanne. Kwa kuwa hawakuweza kumfikisha kwa Yesu kwa sababu ya umati wa watu, walitoboa tundu kwenye paa juu ya mahali Yesu alikuwa, wakamshusha mtu aliyepooza akiwa amelalia mkeka wake. Yesu alipoiona imani yao, alimwambia yule mtu aliyepooza, “Mwanangu, dhambi zako zimesamehewa.”

Video zinazohusiana