Chapa ya Youversion
Ikoni ya Utafutaji

Yohana 5:41-47

Yohana 5:41-47 NEN

“Mimi sitafuti kutukuzwa na wanadamu. Lakini ninajua kwamba hamna upendo wa Mungu mioyoni mwenu. Mimi nimekuja kwa jina la Baba yangu, nanyi hamnipokei, lakini mtu mwingine akija kwa jina lake mwenyewe, mtampokea. Ninyi mwawezaje kuamini ikiwa mnapeana utukufu ninyi kwa ninyi, lakini hamna bidii kupata utukufu utokao kwa Mungu? “Lakini msidhani kuwa mimi nitawashtaki mbele za Baba, mshtaki wenu ni Mose, ambaye mmemwekea tumaini lenu. Kama mngelimwamini Mose, mngeliniamini na mimi kwa maana aliandika habari zangu. Lakini ikiwa hamwamini aliyoandika Mose, mtaaminije ninayoyasema?”

Mipango ya Kusoma Bila Malipo na Ibada zinazohusiana na Yohana 5:41-47

YouVersion hutumia vidakuzi kubinafsisha matumizi yako. Kwa kutumia tovuti yetu, unakubali matumizi yetu ya vidakuzi kama ilivyoelezwa katika Sera yetu ya Faragha