Chapa ya Youversion
Ikoni ya Utafutaji

Yeremia 47

47
Ujumbe kuhusu Wafilisti
1 Hili ndilo neno la Bwana lililomjia nabii Yeremia kuhusu Wafilisti, kabla Farao hajaishambulia Gaza:
2 Hili ndilo asemalo Bwana:
“Tazama jinsi maji yanavyoinuka huko kaskazini,
yatakuwa mafuriko yenye nguvu sana.
Yataifurikia nchi na vitu vyote vilivyo ndani yake,
miji na wanaoishi ndani yake.
Watu watapiga kelele;
wote wanaoishi katika nchi wataomboleza
3 kwa sauti ya kwato za farasi wanaoenda mbio,
kwa sauti ya magari ya vita ya adui,
na mngurumo wa magurudumu yake.
Baba hawatageuka kuwasaidia watoto wao,
mikono yao italegea.
4 Kwa maana siku imewadia
kuwaangamiza Wafilisti wote
na kuwakatilia mbali walionusurika wote
ambao wangeweza kusaidia Tiro na Sidoni.
Bwana anakaribia kuwaangamiza Wafilisti,
mabaki toka pwani za Kaftori#47:4 yaani Krete.
5 Gaza atanyoa kichwa chake katika kuomboleza,
Ashkeloni atanyamazishwa.
Enyi mabaki kwenye tambarare,
mtajikatakata wenyewe hadi lini?
6 “Mnalia, ‘Aa, upanga wa Bwana,
utaendelea hadi lini ndipo upumzike?
Rudi ndani ya ala yako;
acha na utulie.’
7 Lakini upanga utatuliaje
wakati Bwana ameuamuru,
wakati ameuagiza kuishambulia Ashkeloni
pamoja na pwani yake?”

Iliyochaguliwa sasa

Yeremia 47: NEN

Kuonyesha

Nakili

Linganisha

Shirikisha

None

Je, ungependa vivutio vyako vihifadhiwe kwenye vifaa vyako vyote? Jisajili au ingia