Chapa ya Youversion
Ikoni ya Utafutaji

Mhubiri 3:1-11

Mhubiri 3:1-11 NEN

Kuna wakati kwa ajili ya kila jambo, nayo majira kwa kila tendo chini ya mbingu: wakati wa kuzaliwa na wakati wa kufa, wakati wa kupanda na wakati wa kungʼoa yaliyopandwa, wakati wa kuua na wakati wa kuponya, wakati wa kubomoa, na wakati wa kujenga, wakati wa kulia na wakati wa kucheka, wakati wa kuomboleza na wakati wa kucheza, wakati wa kutawanya mawe na wakati wa kukusanya mawe, wakati wa kukumbatia na wakati wa kutokumbatia, wakati wa kutafuta na wakati wa kupoteza, wakati wa kuweka na wakati wa kutupa, wakati wa kurarua na wakati wa kushona, wakati wa kunyamaza na wakati wa kuzungumza, wakati wa kupenda na wakati wa kuchukia, wakati wa vita na wakati wa amani. Mfanyakazi anapata faida gani kutokana na taabu yake? Nimeona mzigo Mungu alioweka juu ya wanadamu. Amefanya kila kitu kiwe kizuri kwa wakati wake. Pia ameiweka hiyo milele katika mioyo ya wanadamu, wala hawawezi kutambua kwa kina yale ambayo Mungu amefanya tangu mwanzo hadi mwisho.

Mipango ya Kusoma Bila Malipo na Ibada zinazohusiana na Mhubiri 3:1-11

YouVersion hutumia vidakuzi kubinafsisha matumizi yako. Kwa kutumia tovuti yetu, unakubali matumizi yetu ya vidakuzi kama ilivyoelezwa katika Sera yetu ya Faragha