2 Yohana Utangulizi
Utangulizi
Waraka wa pili wa Yohana uliandikwa kwa mama mteule na watoto wake. Unaweza kuwa ulimhusu mtu binafsi na jamaa yake, au ulilihusu kanisa fulani. Msisitizo unawekwa katika umuhimu wa imani kwamba Yesu ni Mwana wa Mungu katika umbo la mwanadamu. Inawapasa waumini wanaosoma kudumu katika pendo la Mungu, na kukataa mafundisho mapotovu yanayopinga imani ya kweli.
Yohana pia aliandika kuwaonya ili waweze kutambua walimu wa uongo waliosafiri kila mahali, wasije wakawaunga mkono na kuwasaidia. Yaani mtu yeyote asije akachangia kwenye kueneza mafundisho ya uongo badala ya yale ya kweli.
Mwandishi
Mtume Yohana.
Kusudi
Kuhimiza mwenendo wa muumini, na maonyo kuhusu walimu wa uongo na mbinu zao.
Mahali
Efeso.
Tarehe
Mnamo 90 B.K.
Wahusika Wakuu
Yohana, mama mteule na watoto wake.
Wazo Kuu
Mtume Yohana anaagiza watu kuenenda katika kweli na kumtii Mungu, wakijihadhari na walimu wa uongo, ili wapate kumpenda Mungu, na kupendana wao kwa wao.
Mambo Muhimu
Pendo la kweli ni kuwajali wengine. Tunatamani kupendwa na kuwapenda wengine, lakini tunaona mifano michache sana ya uhalisi katika jambo hili. Dunia imejaa ubinafsi, uchoyo na kujipenda mwenyewe.
Yaliyomo
Salamu (1‑3)
Kweli na upendo (4‑11)
Salamu za mwisho (12‑13).
Iliyochaguliwa sasa
2 Yohana Utangulizi: NENO
Kuonyesha
Shirikisha
Nakili

Je, ungependa vivutio vyako vihifadhiwe kwenye vifaa vyako vyote? Jisajili au ingia
Neno: Biblia Takatifu™ Neno™
Hakimiliki © 1984, 1989, 2009, 2015, 2025 na Biblica, Inc.
Imetumiwa kwa ruhusa. Haki zote zimehifadhiwa duniani kote.
Kiswahili Contemporary Version™
Copyright © 1984, 1989, 2009, 2015, 2025 by Biblica, Inc.
Used with permission. All rights reserved worldwide.