Nalo hilo fungu la tatu nitalitia motoni, niwang'aze kwa kuwayeyusha, kama watu wanavyong'aza fedha kwa kuiyeyusha, tena nitawajaribu kabisa, kama watu wanavyojaribu dhahabu. Kisha hapo, watakapolililia Jina langu, mimi nitawaitikia na kuwaambia: Hawa ndio walio ukoo wangu; ndipo, watakapoitikia wao: Nawe Bwana ndiwe Mungu wetu.