1
Rom 12:2
BIBLIA Yenye Vitabu vya Deuterokanoni HABARI NJEMA
SCLDC10
Msiige mitindo ya ulimwengu huu, bali Mungu afanye mabadiliko ndani yenu kwa kuzigeuza fikira zenu. Hapo ndipo mtakapoweza kuyajua mapenzi ya Mungu na kutambua jambo lililo jema, linalompendeza na kamilifu.
Linganisha
Chunguza Rom 12:2
2
Rom 12:1
Kwa hiyo, ndugu zangu, maadamu Mungu ni mwenye huruma nyingi, nawasihi kwa moyo wote: Mtoleeni Mungu miili yenu kama tambiko iliyo hai, takatifu na yenye kupendeza. Hii ndiyo njia yenu halisi ya kumwabudu.
Chunguza Rom 12:1
3
Rom 12:12
Tumaini lenu liwaweke daima wenye furaha; muwe na saburi katika shida, na kusali daima.
Chunguza Rom 12:12
4
Rom 12:21
Usikubali kushindwa na ubaya, bali ushinde ubaya kwa wema.
Chunguza Rom 12:21
5
Rom 12:10
Pendaneni kindugu; kila mmoja amfikirie kwanza mwenzake kwa heshima.
Chunguza Rom 12:10
6
Rom 12:9
Mapendo yenu na yawe bila unafiki wowote. Chukieni jambo lolote ovu, zingatieni jema.
Chunguza Rom 12:9
7
Rom 12:18
Kadiri inavyowezekana kwa upande wenu, muwe na amani na watu wote.
Chunguza Rom 12:18
8
Rom 12:19
Wapenzi wangu, msilipize kisasi, bali mwachieni Mungu jambo hilo; maana Maandiko Matakatifu yasema: “Kulipiza kisasi ni shauri langu; mimi nitalipiza, asema Bwana.”
Chunguza Rom 12:19
9
Rom 12:11
Msilegee katika bidii, ila muwe wachangamfu rohoni katika kumtumikia Bwana.
Chunguza Rom 12:11
10
Rom 12:3
Kutokana na neema aliyonijalia Mungu, nawaambieni nyinyi nyote: Msijione kuwa ni kitu zaidi kuliko mnavyopaswa kuwa. Fikira zenu na ziwe na kiasi kadiri ya kipimo cha imani Mungu aliyomgawia kila mmoja.
Chunguza Rom 12:3
11
Rom 12:17
Msilipe ovu kwa ovu. Zingatieni mambo mema mbele ya wote.
Chunguza Rom 12:17
12
Rom 12:16
Ishini kwa kupatana vema nyinyi kwa nyinyi. Msijitakie makuu, bali jishughulisheni na madogo. Msijione kuwa wenye hekima sana.
Chunguza Rom 12:16
13
Rom 12:20
Zaidi ya hayo, Maandiko yasema: “Adui yako akiwa na njaa, mpe chakula; akiwa na kiu, mpe kinywaji. Maana kwa kufanya hivyo utamfanya apate aibu kali kama makaa ya moto juu ya kichwa chake.”
Chunguza Rom 12:20
14
Rom 12:14-15
Watakieni baraka wote wanaowadhulumu nyinyi; naam, watakieni baraka na wala msiwalaani. Furahini pamoja na wenye kufurahi, lieni pamoja na wenye kulia.
Chunguza Rom 12:14-15
15
Rom 12:13
Wasaidieni watu wa Mungu katika mahitaji yao; wapokeeni wageni kwa ukarimu.
Chunguza Rom 12:13
16
Rom 12:4-5
Mwili una viungo vingi, kila kimoja na kazi yake. Hali kadhalika ingawa sisi ni wengi, tu mwili mmoja kwa kuungana na Kristo, na kila mmoja ni kiungo cha mwenzake.
Chunguza Rom 12:4-5
Nyumbani
Biblia
Mipango
Video