INJILI ULIMWENGUNI - SEHEMU YA NANEਨਮੂਨਾ

MFANO WA MSAMARIA MWEMA
25 Wakati huo mtaalamu mmoja wa sheria alisimama ili kumjaribu Yesu, akamwuliza,
“Mwalimu, nifanye nini ili nipate kurithi uzima wa milele?”
Yesu akamjibu, “Imeandikwaje katika Torati? Kwani unasoma nini humo?”
Akajibu,
‘Mpende Bwana Mungu wako kwa moyo wako wote, kwa roho yako yote, kwa nguvu zako zote na kwa akili zako zote, tena mpende jirani yako kama unavyojipenda mwenyewe.’ ”
Yesu akamwambia, “Umejibu vyema. Fanya hivyo nawe utaishi.”
Lakini yule mtaalamu wa sheria akitaka kuonyesha kuwa mwenye haki, akamwuliza Yesu, “Jirani yangu ni nani?”
Yesu akamjibu akasema, “Mtu mmoja alikuwa akitelemka kutoka Yerusalemu kwenda Yeriko, naye akaangukia mikononi mwa wanyang'anyi, wakampiga,
wakaondoka, wakamwacha karibu ya kufa.
Kwa bahati nzuri kuhani mmoja alikuwa anapitia njia ile, alipomwona huyo mtu, akapita upande mwingine, akamwacha hapo barabarani.
Vivyo hivyo Mlawi mmoja naye alipofika mahali pale, alimwona, akapita upande mwingine, akamwacha hapo barabarani
Lakini Msamaria mmoja aliyekuwa akisafiri kupitia njia hiyo alipomwona, alimhurumia,
akamwendea, akasafisha majeraha yake kwa divai na mafuta, kisha akayafunga.
Ndipo akampandisha kwenye punda wake akamleta mpaka kwenye nyumba ya wageni na kumtunza.
Kesho yake, yule Msamaria akachukua dinari mbili akampa yule mwenye nyumba ya wageni na kusema, ‘Mtunze, nami nirudipo nitakulipa gharama yo yote ya ziada uliyotumia kwa ajili yake.’
“Ni yupi basi miongoni mwa hawa watatu, wewe unadhani ni jirani yake yule mtu aliyeangukia mikononi mwa wanyang'anyi?”
Yule mtaalamu wa sheria akajibu, “Ni yule aliyemhurumia.”
Ndipo Yesu akamwambia, “Nenda, ukafanye vivyo hivyo.”
ਪਵਿੱਤਰ ਸ਼ਾਸਤਰ
About this Plan

Mfuatano huu ni kusanyiko la hadithi kuhusu maisha Kristo itakayoshirikisha watazamaji wote ulimwenguni kwa kutumia mchanganyiko wa kuona na sauti. Maisha na mafundisho ya Yesu yalidhihirishwa katika kitabu hiki cha hadithi ambacho kinafuata masimulizi ya Agano Jipya yanayopatikana katika vitabu vya Injili vya Mathayo, Marko, Luka, na Yohana
More
Related Plans

Lessons From Ezra

Arid Hearts Lush Hearts

Missionaries in the Marketplace

How to Know Jesus Personally – Start Your Faith Journey Today

A Christian Parent's Guide to Navigating Youth Sports

Connect With God Through Expression | 7-Day Devotional

10 F-Words for the Faith-Driven Entrepreneur

Pray, Lament, Worship and Repent With Psalm 25

Is There Hope for My Marriage? One Good Reason to Stay Together
