INJILI ULIMWENGUNI - SEHEMU YA NANEਨਮੂਨਾ

MWANAMKE ALIYEFUMANIWA AKIZINI
Lakini Yesu akaenda katika Mlima wa Mizeituni.
Alfajiri na mapema Yesu akaja tena Hekaluni, watu wote wakakusanyika, akakaa akaanza kuwafundisha.
"Walimu wa sheria na Mafarisayo wakamleta mwanamke mmoja aliyefumaniwa akizini. Wakamsimamisha katikati ya umati wa watu wote.Wakamwambia Yesu,"
"“Mwalimu, huyu mwanamke amekutwa akizini.Katika sheria, Mose alituamuru kuwapiga kwa mawe wanawake wa namna hii, mpaka wafe. Sasa wewe wasemaje?”"
Walimwuliza swali hili kama mtego ili wapate sababu ya kumshtaki.
Lakini Yesu akainama akaanza kuandika ardhini kwa kidole chake.Walipoendelea kumwulizauliza akainuka, akawaambia,
“Kama kuna mtu ye yote miongoni mwenu ambaye hana dhambi na awe wa kwanza kumtupia jiwe.”
Akainama tena na kuandika ardhini.
Waliposikia haya, wakaanza kuondoka mmoja mmoja, wakianzia wazee, hadi Yesu akabaki peke yake na yule mwanamke akiwa amesimama mbele yake.
Yesu akainuka na kumwambia, “Wako wapi wale waliokuwa wanakuhukumu kuwa mwenye hatia?”
Yule mwanamke akajibu, “Hakuna hata mmoja Bwana.”
Yesu akamwambia, “Hata mimi sikuhukumu. Nenda zako, kuanzia sasa usitende dhambi tena.”
ਪਵਿੱਤਰ ਸ਼ਾਸਤਰ
About this Plan

Mfuatano huu ni kusanyiko la hadithi kuhusu maisha Kristo itakayoshirikisha watazamaji wote ulimwenguni kwa kutumia mchanganyiko wa kuona na sauti. Maisha na mafundisho ya Yesu yalidhihirishwa katika kitabu hiki cha hadithi ambacho kinafuata masimulizi ya Agano Jipya yanayopatikana katika vitabu vya Injili vya Mathayo, Marko, Luka, na Yohana
More
Related Plans

Pursue, Overtake & Recover All

Conversational Evangelism: How to Respond to 7 Common Questions From Nonbelievers

Chunky Blankets & Deep Breaths

Meaningful Work in Seasons of Transition

Good News at Rock Bottom: A 5-Day Devotional Plan With Ray Ortlund

When God Turns It Around: Hope for Hard Times

Storm Watch

Imitators of God

Keys to Answered Prayer
