Logo YouVersion
Îcone de recherche

Mwanzo UTANGULIZI

UTANGULIZI
Kitabu cha Mwanzo ndicho cha kwanza katika orodha ya vitabu vya Biblia. Jina Mwanzo linatokana na kitabu chenyewe (1:1) kwa maana ya asili na chanzo cha ulimwengu, mtu, dhambi, kifo na taifa la Israeli. Jambo la msingi ni Mungu na mtu katika uhusiano wao na pia mpango wa Mungu wa wokovu na uteule wa watu wa wake.
Mungu ndiye Muumba wa vitu vyote. Mungu alimwumba mwanadamu, lakini mwanadamu huyo alimwasi Muumba wake, na kwa uasi wake watu wote wakawa wenye dhambi. Matokeo ya dhambi yakawa kifo. Kwa kuwa tangu mwanzo Mungu aliahidi kuujalia uumbaji wake baraka zake. Ndipo hata mtu alipoasi, Mungu aliendelea kujifunua kwake, kunena na wateule wake, kuwapa wajibu na kuwabariki.
Yaliyomo:
1. Simulizi la awali kuhusu ulimwengu na mtu, Sura 1–11
(a) Kuumba ulimwengu (1–2)
(b) Uasi na kuanguka kwa mtu (3)
(c) Uasi unaongezeka (4–5)
(d) Nuhu na gharika (6–9)
(e) Mnara wa Babeli (10–11)
2. Historia ya awali ya Waisraeli, Sura 12–50
(a) Habari za Abrahamu na watoto wake (12–24)
(b) Habari za Yakobo (25–36)
(c) Habari za Yusufu (37–50)

Sélection en cours:

Mwanzo UTANGULIZI: RSUVDC

Surbrillance

Partager

Copier

None

Tu souhaites voir tes moments forts enregistrés sur tous tes appareils? Inscris-toi ou connecte-toi

YouVersion utilise des cookies pour personnaliser votre expérience. En utilisant notre site Web, vous acceptez l'utilisation des cookies comme décrit dans notre Politique de confidentialité