Soma Biblia Kila Siku 08/2024预览

Mungu ni wa ukweli. Kwa hiyo neno lake ni kweli na uzima, kama Yesu anavyosema katika Yn 6:63,Roho ndiyo itiayo uzima, mwili haufai kitu; maneno hayo niliyowaambia ni roho, tena ni uzima. Vilevile mafundisho yasiyoambatana nalo ni uzushi na uongo. Kwa hiyo Mtume Paulo anamwagiza Timotheo awakataze wenye mafundisho yasiyo kweli ya Mungu. Kwa sababumwisho wa agizo hilo ni upendo utokao katika moyo safi na dhamiri njema(m.5) naMungu ni upendo(1 Yoh 4:16, basi Timotheo afanye anavyoagizwa kwa upendo. Lengo kuu ni watu wasipotoshwe na hadithi zisizoleta uzima, bali waokolewe. Tusiache kuambiana neno la Mungu litupalo uzima, tukikumbuka mambo haya matatu:Moyo safi,dhamiri njemanaimani isiyo na unafiki(m.5).
读经计划介绍

Soma Biblia Kila Siku 08/2024 ni mpango mzuri wa kusoma Biblia kila siku sehemu kwa sehemu kwa mwezi wa Nane pamoja na maelezo mafupi ya kukusaidia kutafakari somo ulilosoma. Katika mpango huu utasoma zaidi kitabu cha 2 Wafalme na 1 Timotheo. Karibu kujiunga na mpango huu
More