Soma Biblia Kila Siku 05/2024预览

Soma Biblia Kila Siku 05/2024

31天中的第23天

Moja ya vikwazo vinavyoweza kuzuia tusiishi maisha matakatifu ya kila siku ni kukosa subira. Binadamu anasahau usemi huu, “Subira yavuta heri”. Waisraeli waliagizwa kumsubiri Mungu. Wakati Musa alipopanda mlimani kwa Mungu na kubaki pale siku 40, alisema:Tungojeeni hapa, mpaka tutakaporudi kwenu(Kut 24:14). Sisi tunaagizwa vivyo hivyo. Waisraeli waliamua kujifanyia mungu mwingine, lakini hakuna mbadala wa Bwana. Kiburi na kujitafutia sifa za watu kunaangusha taifa na kunazaa hali ya kujiundia miungu ya dunia. Tafakari amri ya kwanza:Mimi ni Bwana Mungu wako, usiwe na miungu mingine ila mimi.

读经计划介绍

Soma Biblia Kila Siku 05/2024

Soma Biblia Kila Siku 05/2024 ni mpango mzuri wa kusoma Biblia kila siku sehemu kwa sehemu kwa mwezi wa tano pamoja na maelezo mafupi ya kukusaidia kutafakari somo ulilosoma. Katika mpango huu utasoma zaidi kitabu cha Kutoka, Yoeli na Mathayo. Karibu kujiunga na mpango huu

More