Soma Biblia Kila Siku Juni/2022预览

Wakristo wamefungamanishwa katika umoja wa Roho Mtakatifu, ambaye huwawezesha kuombeana, kutiana moyo, kusaidiana, huku wakikubaliana katika mambo yote, kwa kuhurumiana na kutumikiana. Wakidumu hivyo, kwa nguvu na uweza wa Roho akaaye ndani yao, wanaepushwa na ubinafsi, na wanavikwa kunyenyekeana na kubebeana mizigo kama Kristo alivyofanya, akafanyika mfano kwao. Kwa hiyo tumtazame Kristo, mwenye kuanzisha na mwenye kutimiza imani yetu, tukitaka kuishi tunavyoonywa na somo la leo.
读经计划介绍

Soma Biblia Kila Siku Juni/2022 ni mpango wa kusoma Biblia sehemu kwa sehemu kila siku kwa mwezi wa Juni pamoja na maelezo mafupi yatakayokusaidia kuelewa kwa urahisi na kuendelea kutafakari neno la Mungu ulilosoma kwa siku husika. Katika mpango huu utasoma zaidi katika kitabu cha Wafilipi na Mwanzo. Karibu kujiunga na mpango huu na usome bure
More