Soma Biblia Kila Siku 06/2020预览

Ayubu anajuta ujinga wake uliokuwa umefunika ufahamu wake. Huko nyuma alijitetea na kujihesabia haki. Hali ya Ayubu ni kawaida yetu sote. Tunapokuwa hatuyaelewi matendo ya Mungu katika maisha yetu, hususani yaliyo kinyume na matakwa yetu, tunajaribiwa kuona Mungu hawezi, au ametupuuza, au ametuacha. Ukweli ni kuwa yeye huona yote, na katika kila analoruhusu liwe kwetu lina kusudi lake jema. Kwa hiyo tuwe na utayari wa kuomba kufunuliwa makusudi yake na kutubu tunapogundua kupungukiwa kwetu.
读经计划介绍

Soma Biblia Kila Siku 06/20 ni mpango mzuri wa kusoma Biblia kila siku sehemu kwa sehemu hasa katika kitabu cha 1 Yohana, Ayubu na Mathayo. Mpango huu una maelezo mafupi yatakayokusaidia kuelewa zaidi Neno la Mungu. Karibu kujiunga na mpango huu
More