Soma Biblia Kila Siku 03/2020预览

Soma Biblia Kila Siku 03/2020

31天中的第28天

Kuhani Mkuu na waandishi walijua kutoka kwenye Torati na Manabii kuwa Mungu angemtuma Masihi wake (= Kristo) kwa ajili ya wokovu wao. Waliagizwa na Musa kwamba wamsikie mtu huyo. Kwa hiyo ni ajabu, viongozi hao walimkataa Yesu. Walimsingizia uongo. Na hata walipopata uthibitisho ya kuwa Yeye ndiye Kristo, hawakuwa tayari kukubali. Walimdhalilisha ili aonekane kuwa mtu asiyefaa. Kwa nini Mwokozi alipatwa na haya yote? Yalikuwa lazima ili awapatie wokovu wote wamwaminio. Umkubali na kumwamini Yeye!

读经计划介绍

Soma Biblia Kila Siku 03/2020

Soma Biblia Kila Siku 03/20 ni mpango mzuri wa kusoma Biblia sehemu kwa sehemu hasa katika kitabu cha 2 Samweli, Mathayo na Zaburi. Mpango huu una maelezo mafupi yatakayokusaidia kuelewa zaidi Neno la Mungu. Karibu kusoma na mpango huu

More