Soma Biblia Kila Siku 2预览

Soma Biblia Kila Siku 2

28天中的第6天

Wakati wa Agano la Kale Mwana wa Mungu alijidhihirisha kama "malaika wa Bwana". Linganisha m.2a na m.4. Maana yake ni kwamba Musa alimwona Kristo, Bwana wetu, kijitini (m.6). Wakati wa Agano la Kale palikuwapo mahali maalumu patakatifu ambapo mtu aliweza kumkaribia Mungu. Sharti lilikuwa kwamba afanye maandalizi maalum asije kufa. Lakini baada ya Kristo kufanyika mwili, kuteswa, kufa na kufufuka si hivyo tena. Sasa twaweza kumwabudu Mungu mahali popote kwa sababu ya ukombozi wa Yesu! Soma Yohana 4:20-24 na Waebrania 10:19-22.

读经计划介绍

Soma Biblia Kila Siku 2

Soma Biblia Kila Siku 2 inakupa mpango wa kusoma Biblia kila siku sehemu kwa sehemu, hasa kutoka Kitabu cha Kutoka na Injili ya Yohana, pamoja na maelezo juu ya somo hilo.

More