Soma Biblia Kila Siku 2预览

Soma Biblia Kila Siku 2

28天中的第5天

Musa aliwasaidia binti za kuhani wa Midiani wasifukuzwe. Musa hakusahauliwa na Mungu, bali Mungu alikuwa na mpango wake naye. Mungu akambariki akapata mke na wana hapo ugenini. M.23 unasema: "kilio cha wana wa Israeli kikafika juu kwa Mungu". Mungu alikuwa amesikia muda wote, lakini kwa wakati huu utimilifu wa Mungu uliwadia. Sasa ulikuwa umetimia wakati wa kuwahukumu Wamisri na wakati wa kuwaokoa wana wa Israeli. M.24-25 yaonyesha kwamba sababu ya Mungu kuokoa ni agano lake la neema.

读经计划介绍

Soma Biblia Kila Siku 2

Soma Biblia Kila Siku 2 inakupa mpango wa kusoma Biblia kila siku sehemu kwa sehemu, hasa kutoka Kitabu cha Kutoka na Injili ya Yohana, pamoja na maelezo juu ya somo hilo.

More