YouVersion
Pictograma căutare

Zaburi 108

108
Zaburi 108
Kuomba msaada dhidi ya adui
(Za 57:7‑11; 60:5‑12)
Wimbo. Zaburi ya Daudi.
1 Ee Mungu, moyo wangu ni thabiti;
nitaimba na kusifu kwa moyo wangu wote.
2 Amka, kinubi na zeze!
Nitayaamsha mapambazuko.
3Nitakusifu wewe, Ee Bwana, kati ya mataifa;
nitaimba habari zako, katika jamaa za watu.
4Kwa maana upendo wako ni mkuu, ni juu kuliko mbingu;
uaminifu wako unazifikia anga.
5Ee Mungu, utukuzwe juu ya mbingu,
utukufu wako na uenee duniani kote.
6 Tuokoe na utusaidie kwa mkono wako wa kuume,
ili wale unaowapenda wapate kuokolewa.
7 Mungu amenena kutoka patakatifu pake:
“Nitaigawa Shekemu kwa ushindi
na kulipima Bonde la Sukothi.
8 Gileadi ni yangu, na Manase ni yangu;
Efraimu ni chapeo yangu,
nayo Yuda ni fimbo yangu ya utawala.
9Moabu ni sinia langu la kunawia,
juu ya Edomu natupa kiatu changu;
nashangilia kwa kushindwa kwa Ufilisti.”
10Ni nani atakayenipeleka hadi mji wenye ngome?
Ni nani atakayeniongoza hadi nifike Edomu?
11 Ee Mungu, si ni wewe uliyetukataa sisi,
na hutoki tena na majeshi yetu?
12Tuletee msaada dhidi ya adui,
kwa maana msaada wa mwanadamu haufai kitu.
13Kwa msaada wa Mungu tutapata ushindi,
naye atawaponda adui zetu.

Selectat acum:

Zaburi 108: NEN

Evidențiere

Copiază

Compară

Împărtășește

None

Dorești să ai evidențierile salvate pe toate dispozitivele? Înscrie-te sau conectează-te