YouVersion Logo
Search Icon

Zaburi 2

2
Mfalme mteule wa Mungu
1 # Taz Mate 4:25-26 Kwa nini mataifa yanafanya ghasia?
Mbona watu wanafanya njama za bure?
2Wafalme wa dunia wanajitayarisha;
watawala wanashauriana pamoja,
dhidi ya Mwenyezi-Mungu na mteule wake.
3Wanasema: “Tujiondoe katika utawala wao;
tutupilie mbali minyororo yao!”
4Mwenyezi-Mungu atawalaye juu mbinguni,
anawacheka na kuwadhihaki.
5Kisha, anawakaripia kwa ghadhabu,
na kuwatisha kwa hasira, akisema:
6“Nimemtawaza mfalme niliyemteua,
anatawala Siyoni, mlima wangu mtakatifu!”
7 # Taz Mate 13:33; Ebr 1:5; 5:5 Mfalme asema: “Nitatangaza azimio la Mwenyezi-Mungu.#2:7 Kwanza wafalme wanasema (aya ya 3), pili Mwenyezi-Mungu anasema (aya ya 6), tatu mfalme mteule anasema (aya ya 7).
Mungu aliniambia:
‘Wewe ni mwanangu,
mimi leo nimekuwa baba yako.
8Niombe nami nitakupa mataifa yawe urithi wako,
na dunia nzima kuwa mali yako.
9 # Taz Ufu 2:26,27; 12:5; 19:15 Utawaponda kwa fimbo ya chuma;
utawavunja kama chungu cha mfinyanzi!’”
10Sasa enyi wafalme, tumieni busara;
sikilizeni onyo hili, enyi watawala wa dunia.
11Mtumikieni Mwenyezi-Mungu kwa uchaji;
12msujudieni na kutetemeka;#2:12 msujuduni … kutetemeka: Kiebrania: Mbusuni mwana kwa kutetemeka. Lakini maana yake si dhahiri.
asije akakasirika, mkaangamia ghafla;
kwani hasira yake huwaka haraka.
Heri yao wote wanaokimbilia usalama kwake!

Currently Selected:

Zaburi 2: BHND

Highlight

Share

Copy

None

Want to have your highlights saved across all your devices? Sign up or sign in

YouVersion uses cookies to personalize your experience. By using our website, you accept our use of cookies as described in our Privacy Policy