YouVersion Logo
Search Icon

Malaki 3

3
Watu si waaminifu kwa Mungu
1Yawe wa majeshi anasema: Ninamutuma mujumbe wangu anitangulie kunitengenezea njia. Bwana munayemutafuta atalifikia hekalu lake kwa rafla. Mujumbe munayemutazamia kwa hamu kubwa atakuja na kutangaza agano langu. #Ang. Mat 11.10; Mk 1.2; Lk 1.76; 7.27
2Lakini ni nani atakayevumilia siku ile atakapokuja? Ni nani atakayesimama kuvumilia atakapotokea? Yeye ni kama moto mukali unaosafisha chuma; ni kama sabuni ya mwenye kufua nguo. #Ang. Yoe 2.11; Ufu 6.17 3Yeye atakuja kuhukumu kama mutu anayesafisha na kutakasa feza. Atawasafisha wazao wa Lawi, kama mutu anavyofua zahabu au feza, mpaka wamutolee Yawe sadaka zinazokubalika. 4Hivyo, sadaka za watu wa Yuda na wa Yerusalema zitamupendeza Yawe kama za watu wa zamani; kama katika miaka iliyopita.
5Yawe wa majeshi anasema: Kisha nitawakaribia kwa kuwahukumu. Sitasita kutoa ushuhuda juu ya wachawi, wazinzi, watoa ushuhuda wa uongo, wanaopunja mushahara wa watumishi, wanaowatesa wajane na wayatima, wanaozuia mugeni asipate haki yake na wale wasioniogopa mimi.
Zaka na sadaka
6Yawe wa majeshi alisema hivi: Mimi Yawe sibadiliki. Ni kwa sababu hii, ee ninyi wazao wa Yakobo, hamujateketezwa. 7Tangu wakati wa babu zenu, mumeyazarau masharti yangu wala hamukuyafuata. Munirudilie, nami nitawageukia. Lakini ninyi munaniuliza: Tutakurudilia namna gani?
8Ninawajibia hivi: Ni sawa kwa mutu kumudanganya Mungu? Hapana! Lakini ninyi munanidanganya! Ingawa hivyo ninyi munauliza: Tunakudanganya kwa namna gani? Kweli! Munanidanganya juu ya zaka na sadaka zenu. 9Ninyi na taifa lenu lote mumelaaniwa kwa sababu ya kunidanganya. 10Mulete katika gala yangu zaka yote, kusudi katika nyumba yangu kuwe chakula cha kutosha. Kisha munaweza kunijaribu. Munipime namna hiyo nanyi mutaona kama sitayafungua madirisha ya mbinguni na kuwatiririshia baraka tele. #Ang. Law 27.30; Hes 18.21-24; Kumb 12.5-7; 14.22-29; Neh 13.12 11Wadudu waharibifu nitawazuia wasiyaharibu tena mazao yenu. Mizabibu yenu katika mashamba haitaacha kuzaa matunda. 12Halafu mataifa yote yatawaita ninyi watu waliobarikiwa, maana inchi yenu itakuwa inchi ya furaha. –Ni Yawe, Mungu Mukubwa anayesema hivyo.
13Yawe anasema hivi: Maneno yenu yamekuwa muzigo kwangu. Hata hivyo munasema: Tumesema nini juu yako? 14Ninyi mumesema: Kumutumikia Mungu hakuna faida. Kuna faida gani kuyatii maagizo ya Yawe wa majeshi, au kujaribu kumwonyesha kwamba tumekosa mbele yake kwa kutembea kama watu wanaoomboleza? 15Tunayoona sisi, ni kwamba wenye kiburi ndio wenye furaha siku zote. Watu waovu, ingawa wanastawi, hata wanapomujaribu Mungu, hawapati azabu.
16Halafu watu wanaomutii Yawe walizungumuza wao kwa wao, naye Yawe akasikia mazungumuzo yao. Mbele yake kukawekwa kitabu ambamo uliandikwa ukumbusho wa wale wanaomutii na kumuheshimu. 17Kisha Yawe wa majeshi akasema hivi: Hao watakuwa watu wangu. Watakuwa urizi wangu wa kipekee siku ile nitakaposimama kufanya jambo ninalokusudia. Sitawazuru kama vile baba asivyomuzuru mwana wake anayemutumikia. 18Pale ndipo mutakapotambua tena tofauti inayokuwa kati ya wenye haki na waovu, kati ya mutu anayemutumikia Mungu na asiyemutumikia.
Siku ya Yawe inakuja
19Yawe wa majeshi anasema hivi: Siku inakuja, nayo inawaka kama furu. Wenye kiburi na waovu wote watatupwa mule na kuteketezwa kama majani yenye kukauka; watateketea kabisa wala hakutabaki hata kitambulisho. 20Lakini kwa ajili yenu ninyi munaonitii, uwezo wangu wa kuokoa utawatokea kama jua linalokuwa na nguvu za uponyaji kwenye mishale yake. Mutatoka mukirukaruka kama wana-ngombe wanapotoka katika zizi lao. 21Siku hiyo mutawakanyagakanyaga waovu, nao watakuwa kama majivu chini ya miguu yenu. –Ni Yawe wa majeshi anayesema hivyo.
22Mukumbuke sheria, masharti na maagizo yangu niliyomwamuru mutumishi wangu Musa kwenye mulima Horebu, kusudi awaamuru watu wote wa Israeli.
23Mbele ya kufika kwa siku ile kubwa na ya kutisha, nitamutuma nabii Elia. #Ang. Mat 11.14; 17.10-13; Mk 9.11-13; Lk 1.17; Yn 1.21 24Nabii Elia atawapatanisha wazazi na watoto wao; kama sivyo, nitakuja na kuiangamiza inchi yenu.

Currently Selected:

Malaki 3: SWC02

Highlight

Share

Copy

None

Want to have your highlights saved across all your devices? Sign up or sign in

YouVersion uses cookies to personalize your experience. By using our website, you accept our use of cookies as described in our Privacy Policy