YouVersion Logo
Search Icon

Oba UTANGULIZI

UTANGULIZI
Maana ya jina Obadia katika lugha ya Kiebrania ni “mtumishi wa BWANA” au “mwabudu BWANA”. Kitabu hiki hakitaji kiliandikwa lini, aidha mwandishi alipoishi sio yakini na mambo kadhaa ya ujumbe wake yanasimuliwa katika vitabu vingine vya manabii.
Ujumbe wa Obadia unahusu taifa la Edomu. Edomu maana yake ni “nyekundu” nalo ni jina aliloitwa Esau, wazao wake na nchi walimoishi (Mwa 36:1, 8-9; 25:15, 30). Kwa kuwa Israeli ilitawala Edomu baadaye Waedomi wakajikomba kulikuweko kutoelewana hata uhasama. Yuda ilipotekwa, Yerusalemu ukabomolewa, wakazi wake wakachukuliwa mateka, Edomu walifurahi wakajiunga na adui ya Yuda kupora mali ya Yuda. Ujumbe wa nabii Obadia unaeleza hali ya uhasama na mafarakano yaliyokuwapo kati ya mataifa ndugu. Pia ukatoa hukumu ya Mungu kwa Edomu. “Siku ya BWANA” ni wakati ambapo taifa la Mungu litalipiza kisasi kwa Edomu.
Yaliyomo:
1. Mungu atashusha kiburi cha Edomu, Aya 1-4
2. Mungu ataangamiza nchi ya Edomu, Aya 5-9
3. Sababu za kuangamizwa Edomu, Aya 10-16
4. Israeli na Yuda wataimarishwa, Aya 17-21

Currently Selected:

Oba UTANGULIZI: SUV

Highlight

Share

Copy

None

Want to have your highlights saved across all your devices? Sign up or sign in

YouVersion uses cookies to personalize your experience. By using our website, you accept our use of cookies as described in our Privacy Policy