Soma Biblia Kila Siku 06/2024预览

Soma Biblia Kila Siku 06/2024

30天中的第10天

Utakuja wakati ambapo watu watayakataa mafundisho ya Neno la Mungu yenye uzima na badala yake kupenda mafundisho ya uongo. Kwa hiyo Paulo anamwagiza Timotheo mbele ya Mungu kufanya kazi ya mhubiri wa Injili. Je, hali ikoje wakati wetu? Neno la Mungu linahubiriwa ipasavyo na watu wote wanapenda mafundisho yake ya kweli? Bila shaka hali ni tofauti. Kama Timotheo, sisi pia tunaagizwa kutahadhari. Tudumu katika imani na kuwa na kiasi na uvumilivu tukihubiri Injilikwa uhodari wote. Bwana yu karibu!

读经计划介绍

Soma Biblia Kila Siku 06/2024

Soma Biblia Kila Siku 06/2024 ni mpango mzuri wa kusoma Biblia kila siku sehemu kwa sehemu kwa mwezi wa sita pamoja na maelezo mafupi ya kukusaidia kutafakari somo ulilosoma. Katika mpango huu utasoma zaidi kitabu cha 2 Timotheo na 2 Wafalme. Karibu kujiunga na mpango huu

More