Soma Biblia Kila Siku 10/2020预览

Soma Biblia Kila Siku 10/2020

31天中的第6天

Ni watu wachache sana wanaojivunia mateso. Hawa ni wale Wakristo waaminifu, walioteswa kwa namna nyingi kwa sababu ya kumshuhudia Yesu Kristo na utawala wake. Wamemfuata Yesu Kristo katika kila hatua ya maisha. Paulo analazimika kuweka bayana mateso yaliyompata. Nia yake si ili kujitwalia sifa na utukufu. La hasha! Mateso yake yanadhihirisha utume wake kuwa umetoka kwa Yesu Kristo. Ukipenda kujifunza zaidi kuhusu mateso ya Paulo na alivyovumilia hayo yote kwa ajili ya Kristo, soma k.m. Flp 3:4-8, Mdo 14:19, 16:22-24, 21:30-33, na 22:24-30.

读经计划介绍

Soma Biblia Kila Siku 10/2020

Soma Biblia Kila Siku 10/20 ni mpango mzuri wa kusoma Biblia kila siku sehemu kwa sehemu hasa katika kitabu cha 2 Wakorintho, Mwanzo na 1 Petro. Mpango huu una maelezo mafupi yatakayokusaidia kuelewa zaidi Neno la Mungu. Karibu kujiunga na mpango huu

More