YouVersion
Pictograma căutare

Zaburi 82

82
Zaburi 82
Maombi kwa ajili ya kutaka haki
Zaburi ya Asafu.
1 Mungu anaongoza kusanyiko kuu,
anatoa hukumu miongoni mwa “miungu”:
2 “Hata lini utaendelea kuwatetea wasio haki
na kuonesha upendeleo kwa waovu?
3 Teteeni wanyonge na yatima,
tunzeni haki za maskini na waliodhulumiwa.
4Mwokoeni mnyonge na mhitaji,
wakomboeni kutoka mkononi mwa mwovu.
5 “Hawajui lolote, hawaelewi lolote.
Wanatembea gizani;
misingi yote ya dunia imetikisika.
6 “Nilisema, ‘Ninyi ni “miungu”;
ninyi nyote ni wana wa Aliye Juu Sana.’
7 Lakini mtakufa kama wanadamu wa kawaida;
mtaanguka kama mtawala mwingine yeyote.”
8 Ee Mungu, inuka uihukumu nchi,
kwa kuwa mataifa yote ni urithi wako.

Selectat acum:

Zaburi 82: NEN

Evidențiere

Copiază

Compară

Împărtășește

None

Dorești să ai evidențierile salvate pe toate dispozitivele? Înscrie-te sau conectează-te