YouVersion
Pictograma căutare

Zaburi 53

53
Zaburi 53
Uovu wa wanadamu
(Za 14)
Kwa mwimbishaji. Mtindo wa mahalathi. Utenzi wa Daudi.
1 Mpumbavu anasema moyoni mwake,
“Hakuna Mungu.”
Wameharibika, na njia zao ni za uovu kabisa,
hakuna hata mmoja atendaye mema.
2 Mungu anawachungulia wanadamu chini
kutoka mbinguni
aone kama wako wenye akili,
wowote wanaomtafuta Mungu.
3 Kila mmoja amegeukia mbali,
wameharibika wote pamoja,
hakuna atendaye mema.
Naam, hakuna hata mmoja!
4 Je, watendao maovu kamwe hawatajifunza:
wale ambao huwala watu wangu
kama watu walavyo mkate,
hao ambao hawamwiti Mungu?
5 Hapo waliingiwa na hofu kuu,
ambapo hapakuwa na hofu.
Mungu alitawanya mifupa ya wale waliokushambulia;
uliwaaibisha, kwa sababu Mungu aliwadharau.
6Laiti wokovu wa Israeli ungekuja kutoka Sayuni!
Mungu anaporejesha wafungwa wa watu wake,
Yakobo na ashangilie, Israeli na afurahi!

Selectat acum:

Zaburi 53: NEN

Evidențiere

Copiază

Compară

Împărtășește

None

Dorești să ai evidențierile salvate pe toate dispozitivele? Înscrie-te sau conectează-te