Zaburi 126
126
Zaburi 126
Kurejeshwa kutoka uhamisho
Wimbo wa kwenda juu.
1 Bwana alipowarejesha mateka Sayuni,
tulikuwa kama watu walioota ndoto.
2 Vinywa vyetu vilijaa kicheko,
ndimi zetu zilijaa nyimbo za shangwe.
Ndipo iliposemwa miongoni mwa mataifa,
“Bwana amewatendea mambo makuu.”
3 Bwana ametutendea mambo makuu,
nasi tumejaa furaha.
4 Ee Bwana, turejeshee watu wetu waliotekwa,
kama vijito katika Negebu.
5 Wapandao kwa machozi
watavuna kwa nyimbo za shangwe.
6Yeye azichukuaye mbegu zake
kwenda kupanda, huku akilia,
atarudi kwa nyimbo za shangwe,
akichukua miganda ya mavuno yake.
Selectat acum:
Zaburi 126: NEN
Evidențiere
Copiază
Compară
Împărtășește
Dorești să ai evidențierile salvate pe toate dispozitivele? Înscrie-te sau conectează-te
Holy Bible, Kiswahili Contemporary Version™ (Neno: Biblia Takatifu™) | Copyright © 1984, 1989, 2009, 2015, 2025 by Biblica, Inc. | Used with permission. All rights reserved worldwide.
Biblica® Cross Reference System | Copyright © 2025 by Biblica, Inc. | Used with permission. All rights reserved worldwide.