Zaburi 124
124
Zaburi 124
Shukrani kwa ukombozi wa Israeli
Wimbo wa kwenda juu. Wa Daudi.
1 Kama Bwana hangekuwa upande wetu;
Israeli na aseme sasa:
2kama Bwana hangekuwa upande wetu,
watu walipotushambulia,
3 hasira yao ilipowaka dhidi yetu,
wangetumeza tukiwa hai,
4 mafuriko yangegharikisha,
maji mengi yangetufunika,
5maji yaendayo kasi
yangetuchukua.
6Ahimidiwe Bwana,
ambaye hakuruhusu turaruliwe kwa meno yao.
7 Tumeponyoka kama ndege
kutoka mtego wa mwindaji;
mtego umevunjika,
nasi tumeokoka.
8 Msaada wetu ni katika jina la Bwana,
Muumba wa mbingu na dunia.
Selectat acum:
Zaburi 124: NEN
Evidențiere
Copiază
Compară
Împărtășește
Dorești să ai evidențierile salvate pe toate dispozitivele? Înscrie-te sau conectează-te
Holy Bible, Kiswahili Contemporary Version™ (Neno: Biblia Takatifu™) | Copyright © 1984, 1989, 2009, 2015, 2025 by Biblica, Inc. | Used with permission. All rights reserved worldwide.
Biblica® Cross Reference System | Copyright © 2025 by Biblica, Inc. | Used with permission. All rights reserved worldwide.