Zaburi 122
122
Zaburi 122
Sifa kwa Yerusalemu
Wimbo wa kwenda juu. Wa Daudi.
1 Nilishangilia pamoja na wale walioniambia,
“Twende nyumbani mwa Bwana.”
2Ee Yerusalemu, miguu yetu imesimama
malangoni mwako.
3 Yerusalemu imejengwa vyema kama mji
ulioshikamana pamoja.
4 Huko ndiko makabila hukwea,
makabila ya Bwana,
kulisifu jina la Bwana kulingana na maagizo
waliopewa Israeli.
5Huko viti vya hukumu hukaa,
viti vya ufalme vya nyumba ya Daudi.
6 Omba kwa ajili ya amani ya Yerusalemu:
“Wote wanaokupenda na wawe salama.
7 Amani na iwe ndani ya kuta zako,
na usalama ndani ya ngome zako.”
8Kwa ajili ya ndugu na rafiki zangu,
nitasema, “Amani iwe ndani yako.”
9 Kwa ajili ya nyumba ya Bwana Mungu wetu,
nitatafuta mafanikio yako.
Selectat acum:
Zaburi 122: NEN
Evidențiere
Copiază
Compară
Împărtășește
Dorești să ai evidențierile salvate pe toate dispozitivele? Înscrie-te sau conectează-te
Holy Bible, Kiswahili Contemporary Version™ (Neno: Biblia Takatifu™) | Copyright © 1984, 1989, 2009, 2015, 2025 by Biblica, Inc. | Used with permission. All rights reserved worldwide.
Biblica® Cross Reference System | Copyright © 2025 by Biblica, Inc. | Used with permission. All rights reserved worldwide.