1
Mathayo 16:24
Agano Jipya: Tafsiri ya Kusoma-Kwa-Urahisi
TKU
Kisha Yesu akawaambia wafuasi wake, “Ikiwa yeyote miongoni mwenu anataka kuwa mfuasi wangu, ni lazima aache kujiwazia yeye mwenyewe na mahitaji yake. Ni lazima awe radhi kuubeba msalaba aliopewa na kunifuata mimi.
Confronta
Esplora Mathayo 16:24
2
Mathayo 16:18
Hivyo ninakwambia, Wewe ni Petro. Na nitalijenga kanisa langu kwenye mwamba huu. Nguvu ya mauti haitaweza kulishinda kanisa langu.
Esplora Mathayo 16:18
3
Mathayo 16:19
Nitawapa funguo za Ufalme wa Mungu. Mnapohukumu hapa duniani, hukumu hiyo itakuwa hukumu ya Mungu. Mnapotamka msamaha hapa duniani, msamaha huo utakuwa msamaha wa Mungu.”
Esplora Mathayo 16:19
4
Mathayo 16:25
Yeyote kati yenu anayetaka kuokoa uhai wake, ataupoteza. Lakini ninyi mlioyaacha maisha yenu kwa ajili yangu mtaupata uzima wa kweli.
Esplora Mathayo 16:25
5
Mathayo 16:26
Haina maana kwenu ninyi kuupata ulimwengu wote, ikiwa ninyi wenyewe mtapotea. Mtu atalipa nini ili kuyapata tena maisha yake baada ya kuyapoteza?
Esplora Mathayo 16:26
6
Mathayo 16:15-16
Kisha Yesu akawauliza, “Na ninyi mnasema mimi ni nani?” Simoni Petro akajibu, “Wewe ni Masihi, Mwana wa Mungu aliye hai.”
Esplora Mathayo 16:15-16
7
Mathayo 16:17
Yesu akajibu, “Umebarikiwa, Simoni mwana wa Yona. Hakuna aliyekufundisha hilo ila Baba yangu wa mbinguni ndiye amekuonesha mimi ni nani.
Esplora Mathayo 16:17