Amosi 6
6
Azabu kwa sababu ya kujiaminia
1Ole kwenu ninyi munaostarehe kule Sayuni,
nanyi munaoishi katika usalama kwenye mulima Samaria!
Ninyi munaonekana kuwa waongozi wa taifa kubwa,
ambao Waisraeli wote wanawategemea.
2Muende Kalne, muangalie.
Tokea kule muende mpaka katika ule muji mukubwa wa Hamati,
kisha mutelemuke mpaka Gati kwa Wafilistini.
Mutatambua kwamba ninyi si bora kuliko falme zile,
hata kama eneo lao ni ndogo zaidi ya lenu.
3Ninyi munajaribu kuifukuza ile siku mbaya.
Lakini munaukaribisha utawala wa mateso.
4Ole kwenu ninyi munaolalia juu ya vitanda vya pembe za tembo
na kujinyoosha juu ya matandiko yao,
mukikula nyama za wana-kondoo na wana-ngombe!
5Ninyi munapenda kuimba ovyo na sauti ya vinubi
na kutunga ala mupya za muziki mukimwiga mufalme Daudi.
6Munakunywa divai katika mabakuli,
na kujipakaa marasi mazuri kabisa.
Lakini hamuhuzuniki hata kidogo
juu ya kuangamia kwa wazao wa Yosefu.
7Kwa hiyo mutakuwa wa kwanza kwenda katika uhamisho,
na karamu za wenye kustarehe zitatoweka.
8Bwana wetu Yawe ameapa kwa nafsi yake:
Ninachukizwa sana na kiburi cha wazao wa Yakobo;
tena ninachukia nyumba zao nzuri sana.
–Ni ujumbe wa Yawe.–
Muji wao na vyote vinavyokuwa ndani yake nitavipatia waadui zake.
9Kama wakibaki watu kumi katika nyumba moja, wote watakufa. 10Na mujomba wa yule aliyekufa atakapokuja kuitoa maiti inje aichome, akimwuliza yeyote atakayekuwa ndani pembeni ya nyumba: Kuna mutu mwingine pamoja nawe? Atajibiwa: Hakuna! Naye atamwambia: Nyamaza kimya! Tusilitaje hata jina la Yawe.
11Yawe anatoa amri,
na nyumba kubwa inabomoka vipandevipande,
na nyumba ndogo kusagikasagika.
12Farasi wanaweza kukimbia katika mawe makubwa?
Watu wanaweza kulima bahari na ngombe?
Lakini ninyi mumeigeuza sheria kuwa sumu,
na tunda la haki kuwa uchungu.
13Ninyi munashangilia juu ya muji wa Bure#6.13 Bure: ni maana ya jina Lodebari.
na kusema mumeuteka muji wa Nguvu#6.13 Nguvu: Katika kiebrania, jina la muji huu mudogo ni “pembe” nazo ni kitambulisho cha nguvu. kwa nguvu zenu wenyewe.
14Enyi Waisraeli,
kweli nitaleta taifa moja likuje kuwashambulia.
–Ni ujumbe wa Yawe.–
Nalo litawatesa ninyi kuanzia Hamati upande wa kaskazini,
mpaka kwenye kijito cha Araba, upande wa kusini.
Nke Ahọpụtara Ugbu A:
Amosi 6: SWC02
Mee ka ọ bụrụ isi
Kesaa
Lee anya n'etiti ihe abụọ
Mapịa
Ịchọrọ ka echekwaara gị ihe ndị gasị ị mere ka ha pụta ìhè ná ngwaọrụ gị niile? Debanye aha gị ma ọ bụ mee mbanye
Bible in Swahili Congo © Bible Society of the Democratic Republic of Congo (DRC), 2002.