Yoeli UTANGULIZI
UTANGULIZI
Hatujui mengi juu ya mambo yanoyoelekea huyu nabii Yoeli zaidi ya yale tunayoambiwa kwa ufupi sana kwa mwanzo wa kitabu hiki, wala hatuwezi kusema kwa uhakika aliishi nyakati gani.
Mwanzo wa kitabu hiki kinaonyesha namna inchi ilivyoharibiwa na nzige pamoja na kukauka kwa maji. Yoeli anaona na kutangaza kwamba ni kitambulisho cha kuja kwa Siku ya Yawe. Kwake ni wazi kwamba Mungu atakamata mupango wa kuwaazibu wote wanaopinga mapenzi yake.
Yoeli anataka watu warudilie Mungu kikamilifu. Anasema juu ya wakati Mungu atakapowashushia watu wote Roho wake, wanaume na wanawake, watoto na wazee (3.1-5). Katika Agano Jipya ahadi hiyo ya Mungu imepangwa kukamilika kwa kuja kwa Roho Mutakatifu (angalia Matendo 2.17-21).
נבחרו כעת:
Yoeli UTANGULIZI: SWC02
הדגשה
העתק
השווה
שתפו
רוצים לשמור את ההדגשות שלכם בכל המכשירים שלכם? הירשמו או היכנסו
Bible in Swahili Congo © Bible Society of the Democratic Republic of Congo (DRC), 2002.