Λογότυπο YouVersion
Εικονίδιο αναζήτησης

Mwanzo Utangulizi

Utangulizi
Kitabu hiki kiliandikwa kuelezea vile vitu vyote vilianza. Neno “Mwanzo” linatokana na maana ya “asili” au “chanzo.” Kinaelezea kwamba Mwenyezi Mungu aliumba ulimwengu wote, vile mwanadamu aliumbwa na kuwekwa katika mazingira yaliyokuwa kamili, vile dhambi ilianza, na vile Mwenyezi Mungu alitoa wokovu kwa mwanadamu aliyepotea. Mwanzo wa historia ya mwanadamu unaelezewa, mwanzo wa sanaa na mwanadamu kutengeneza vifaa, vile lugha za wanadamu zilianza, na kule mataifa tofauti yalitokea. Kitabu kinaendelea kuelezea chanzo cha Waebrania naye Ibrahimu, akifuatiwa na habari za Isaka, Yakobo na wanawe, na kitabu kinaishia na Yusufu akiwa Misri.
Wazo Kuu
Wazo kuu katika kitabu hiki ni kwamba, ingawa Mwenyezi Mungu aliumba vitu vyote vikiwa vizuri nayo dhambi ya mwanadamu ikaviharibu, Mwenyezi Mungu hajakufa moyo, bali sasa anamtafuta mwanadamu ili kumwokoa. Mamlaka ya Mwenyezi Mungu juu ya mambo yote yanasisitizwa, mtazamo wa kipekee ukiwa vile Mwenyezi Mungu anaendesha historia kuleta wema kwa watu wake na wokovu wao (50:20).
Mwandishi
Musa.
Tarehe
Kama mwaka wa 1420 au 1220 KK.
Mgawanyo
Kuumbwa kwa ulimwengu, na mwanadamu (1:1–2:25)
Kuanguka kwa mwanadamu, na chanzo cha dhambi (3:1–4:26)
Historia ya mwanadamu aliyeanguka hadi gharika (5:1–9:29)
Binadamu kuenea duniani kote (10:1–11:32)
Maisha ya Ibrahimu (12:1–25:18)
Maisha ya Isaka (25:19–26:35)
Maisha ya Yakobo na Esau (27:1–37:1)
Maisha ya Yusufu (37:2–50:26).

Επιλέχθηκαν προς το παρόν:

Mwanzo Utangulizi: NMM

Επισημάνσεις

Κοινοποίηση

Αντιγραφή

None

Θέλετε να αποθηκεύονται οι επισημάνσεις σας σε όλες τις συσκευές σας; Εγγραφείτε ή συνδεθείτε

Η YouVersion χρησιμοποιεί cookies για να εξατομικεύσει την εμπειρία σας. Χρησιμοποιώντας τον ιστότοπό μας, αποδέχεστε τη χρήση των cookies όπως περιγράφεται στην πολιτική απορρήτου