1
Waroma 8:28
Biblia Habari Njema
BHN
Tunajua kwamba, katika mambo yote, Mungu hufanya kazi na kuifanikisha pamoja na wote wampendao, yaani wale aliowaita kadiri ya kusudi lake.
قارن
اكتشف Waroma 8:28
2
Waroma 8:38-39
Maana ninajua hakika kwamba hakuna kitu kiwezacho kututenganisha na upendo wake: Wala kifo, wala uhai; wala malaika au nguvu nyingine za mbinguni; wala yanayotokea sasa, wala yatakayotokea baadaye; wala mamlaka; wala ulimwengu wa juu, wala wa chini kabisa. Hakuna kiumbe chochote kitakachoweza kututenga na upendo wa Mungu katika Kristo Yesu Bwana wetu.
اكتشف Waroma 8:38-39
3
Waroma 8:26
Hali kadhalika, naye Roho anatusaidia katika udhaifu wetu. Maana hatujui inavyotupasa kuomba; lakini Roho mwenyewe anatuombea kwa Mungu kwa mlio wa huzuni usioelezeka.
اكتشف Waroma 8:26
4
Waroma 8:31
Kutokana na hayo, tuseme nini zaidi? Ikiwa Mungu yuko upande wetu, nani awezaye kutupinga?
اكتشف Waroma 8:31
5
Waroma 8:1
Kwa hiyo, sasa hakuna hukumu kwa wale ambao katika maisha yao wameungana na Kristo.
اكتشف Waroma 8:1
6
Waroma 8:6
Fikira za mwili huleta kifo; fikira za Roho huleta uhai na amani.
اكتشف Waroma 8:6
7
Waroma 8:37
Lakini, katika mambo haya yote, tumepata ushindi mkubwa kwa msaada wake yeye aliyetupenda.
اكتشف Waroma 8:37
8
Waroma 8:18
Naona kuwa mateso ya wakati huu wa sasa si kitu kamwe kama tukiyalinganisha na ule utukufu utakaodhihirishwa kwetu.
اكتشف Waroma 8:18
9
Waroma 8:35
Ni nani awezaye kututenga na upendo wa Kristo? Je, ni taabu, au dhiki, au mateso, au njaa, au ukosefu wa nguo, au hatari, au kifo?
اكتشف Waroma 8:35
10
Waroma 8:27
Naye Mungu aonaye mpaka ndani ya mioyo ya watu, anajua fikira ya huyo Roho; kwani huyo Roho huwaombea watu wa Mungu kufuatana na mapenzi ya Mungu.
اكتشف Waroma 8:27
11
Waroma 8:14
Wote wanaoongozwa na Roho wa Mungu ni watoto wa Mungu.
اكتشف Waroma 8:14
12
Waroma 8:5
Maana, wale wanaoishi kufuatana na matakwa ya mwili, hutawaliwa na fikira za mwili. Lakini wale wanaoishi kufuatana na matakwa ya Roho Mtakatifu, hutawaliwa na fikira za Roho.
اكتشف Waroma 8:5
13
Waroma 8:32
Mungu hakumhurumia hata Mwanae wa pekee, bali alimtoa kwa ajili yetu sisi sote. Ikiwa amefanya hivyo, je, hatatujalia pia mema yote?
اكتشف Waroma 8:32
14
Waroma 8:16-17
Naye Roho mwenyewe anathibitisha na roho zetu kwamba sisi ni watoto wa Mungu. Basi, kwa vile sisi ni watoto wa Mungu, tutapokea baraka zote Mungu alizowawekea watu wake, na tutashiriki urithi huo pamoja na Kristo; maana, tukiyashiriki mateso yake Kristo, tutaushiriki pia utukufu wake.
اكتشف Waroma 8:16-17
15
Waroma 8:7
Maana, mwenye kutawaliwa na fikira za mwili ni adui wa Mungu; haitii sheria ya Mungu, wala hawezi kuitii.
اكتشف Waroma 8:7
16
Waroma 8:19
Viumbe vyote vinangojea kwa hamu Mungu awadhihirishe watoto wake.
اكتشف Waroma 8:19
17
Waroma 8:22
Kwa maana tunajua kwamba mpaka hivi sasa, viumbe vyote vinalia kwa maumivu kama ya kujifungua mtoto.
اكتشف Waroma 8:22