1
Rom 8:28
BIBLIA Yenye Vitabu vya Deuterokanoni HABARI NJEMA
SCLDC10
Tunajua kwamba, katika mambo yote, Mungu hufanya kazi na kuifanikisha pamoja na wote wampendao, yaani wale aliowaita kadiri ya kusudi lake.
موازنہ
تلاش Rom 8:28
2
Rom 8:38-39
Maana ninajua hakika kwamba hakuna kitu kiwezacho kututenganisha na upendo wake: Wala kifo, wala uhai; wala malaika au nguvu nyingine za mbinguni; wala yanayotokea sasa, wala yatakayotokea baadaye; wala mamlaka; wala ulimwengu wa juu, wala wa chini kabisa. Hakuna kiumbe chochote kitakachoweza kututenga na upendo wa Mungu katika Kristo Yesu Bwana wetu.
تلاش Rom 8:38-39
3
Rom 8:26
Hali kadhalika, naye Roho anatusaidia katika udhaifu wetu. Maana hatujui inavyotupasa kuomba; lakini Roho mwenyewe anatuombea kwa Mungu kwa mlio wa huzuni usioelezeka.
تلاش Rom 8:26
4
Rom 8:31
Kutokana na hayo, tuseme nini zaidi? Ikiwa Mungu yuko upande wetu, nani awezaye kutupinga?
تلاش Rom 8:31
5
Rom 8:1
Kwa hiyo, sasa hakuna hukumu kwa wale ambao katika maisha yao wameungana na Kristo.
تلاش Rom 8:1
6
Rom 8:6
Fikira za mwili huleta kifo; fikira za Roho huleta uhai na amani.
تلاش Rom 8:6
7
Rom 8:37
Lakini, katika mambo haya yote, tumepata ushindi mkubwa kwa msaada wake yeye aliyetupenda.
تلاش Rom 8:37
8
Rom 8:18
Naona kuwa mateso ya wakati huu wa sasa si kitu kamwe kama tukiyalinganisha na ule utukufu utakaodhihirishwa kwetu.
تلاش Rom 8:18
9
Rom 8:35
Ni nani awezaye kututenga na upendo wa Kristo? Je, ni taabu, au dhiki, au mateso, au njaa, au ukosefu wa nguo, au hatari, au kifo?
تلاش Rom 8:35
10
Rom 8:27
Naye Mungu aonaye mpaka ndani ya mioyo ya watu, anajua fikira ya huyo Roho; kwani huyo Roho huwaombea watu wa Mungu kufuatana na mapenzi ya Mungu.
تلاش Rom 8:27
11
Rom 8:14
Wote wanaoongozwa na Roho wa Mungu ni watoto wa Mungu.
تلاش Rom 8:14
12
Rom 8:5
Maana, wale wanaoishi kufuatana na matakwa ya mwili, hutawaliwa na fikira za mwili. Lakini wale wanaoishi kufuatana na matakwa ya Roho Mtakatifu, hutawaliwa na fikira za Roho.
تلاش Rom 8:5
13
Rom 8:32
Mungu hakumhurumia hata Mwanae wa pekee, bali alimtoa kwa ajili yetu sisi sote. Ikiwa amefanya hivyo, je, hatatujalia pia mema yote?
تلاش Rom 8:32
14
Rom 8:16-17
Naye Roho mwenyewe anathibitisha na roho zetu kwamba sisi ni watoto wa Mungu. Basi, kwa vile sisi ni watoto wa Mungu, tutapokea baraka zote Mungu alizowawekea watu wake, na tutashiriki urithi huo pamoja na Kristo; maana, tukiyashiriki mateso yake Kristo, tutaushiriki pia utukufu wake.
تلاش Rom 8:16-17
15
Rom 8:7
Maana, mwenye kutawaliwa na fikira za mwili ni adui wa Mungu; haitii sheria ya Mungu, wala hawezi kuitii.
تلاش Rom 8:7
16
Rom 8:19
Viumbe vyote vinangojea kwa hamu Mungu awadhihirishe watoto wake.
تلاش Rom 8:19
17
Rom 8:22
Kwa maana tunajua kwamba mpaka hivi sasa, viumbe vyote vinalia kwa maumivu kama ya kujifungua mtoto.
تلاش Rom 8:22