1
Waroma 14:17-18
BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002
SWC02
Kwa maana kazi ya Ufalme wa Mungu si kushugulika na mambo ya kula na kunywa, lakini ni kushugulika na haki, amani na furaha vinavyotolewa na Roho Mutakatifu. Na yeyote anayemutumikia Kristo kwa njia hiyo anamupendeza Mungu, naye anapata kuwa mwenye kustahili mbele ya watu.
موازنہ
تلاش Waroma 14:17-18
2
Waroma 14:8
Maana kama tunaishi, tunaishi kwa ajili ya Bwana, na kama tunakufa, tunakufa kwa ajili ya Bwana. Basi ikiwa tunaishi, au ikiwa tunakufa, sisi ni watu wa Bwana.
تلاش Waroma 14:8
3
Waroma 14:19
Basi kwa hiyo tujikaze sana kufanya mambo yale yanayoleta amani na yanayotusaidia kujengana katika imani.
تلاش Waroma 14:19
4
Waroma 14:13
Basi tusihukumiane tena sisi wenyewe. Lakini tafazali mukamate kusudi hili: mutu asifanye kitu kinachoweza kumukwaza au kumwangusha ndugu yake katika zambi.
تلاش Waroma 14:13
5
Waroma 14:11-12
Kwa maana imeandikwa katika Maandiko Matakatifu: “Bwana anasema: Kama vile ninavyoishi, kila mutu atapiga magoti mbele yangu, na kila mutu ataitikia kwamba mimi ni Mungu.” Kwa hiyo kila mumoja kati yetu atajitetea mwenyewe kwa Mungu.
تلاش Waroma 14:11-12
6
Waroma 14:1
Mumupokee yule anayekuwa zaifu katika imani pasipo kubishana naye juu ya mawazo yake.
تلاش Waroma 14:1
7
Waroma 14:4
Wewe ni nani unayehukumu mutumishi wa mwingine? Akisimama imara katika kazi yake au akianguka, hilo ni shauri la bwana wake. Naye atasimama imara maana Bwana yuko na uwezo wa kumusimamisha.
تلاش Waroma 14:4
صفحہ اول
بائبل
مطالعاتی منصوبہ
Videos