1
Wakolosayi 3:13
BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002
SWC02
Muvumiliane na kusameheana ninyi kwa ninyi wakati wowote mutu anapokuwa na neno la kumushitaki mwingine. Munapaswa kusameheana kama vile Bwana alivyowasamehe ninyi.
موازنہ
تلاش Wakolosayi 3:13
2
Wakolosayi 3:2
Mushugulikie sana mambo yanayokuwa juu, lakini musishugulikie mambo yanayokuwa katika dunia.
تلاش Wakolosayi 3:2
3
Wakolosayi 3:23
Na kila kitu munachofanya, mukifanye kwa moyo wenu wote, kama vile wenye kumutumikia Bwana wala si watu.
تلاش Wakolosayi 3:23
4
Wakolosayi 3:12
Ninyi ni watu wa Mungu, yeye amewapenda na kuwachagua kwa ajili yake mwenyewe. Kwa hiyo, mukuwe na moyo wa huruma, wema, unyenyekevu, upole na uvumilivu.
تلاش Wakolosayi 3:12
5
Wakolosayi 3:16-17
Habari za Kristo zikae ndani yenu kwa uwingi. Mufundishane na mushauriane kwa hekima. Mumwimbie Mungu kwa moyo wenu wote na kumushukuru kwa zaburi na nyimbo za kiroho. Kila kitu munachofanya au kusema, mufanye yote kwa jina la Bwana Yesu, kwa kumushukuru Mungu Baba kwa njia yake.
تلاش Wakolosayi 3:16-17
6
Wakolosayi 3:14
Zaidi ya mambo haya yote, mukuwe na upendo, maana upendo unaunganisha kila kitu katika umoja unaokuwa mukamilifu.
تلاش Wakolosayi 3:14
7
Wakolosayi 3:1
Kwa kuwa mumefufuliwa pamoja na Kristo, mutafute mambo yanayokuwa juu, pahali Kristo anapoikaa na mamlaka kwa kuume kwa Mungu.
تلاش Wakolosayi 3:1
8
Wakolosayi 3:15
Amani ya Kristo itawale katika mioyo yenu; maana ni kwa ajili ya hiyo ninyi mumeitwa kuwa katika mwili mumoja. Mukuwe wenye shukrani.
تلاش Wakolosayi 3:15
9
Wakolosayi 3:5
Basi mutupilie mbali mambo yote ya kidunia yanayokuwa ndani yenu: uasherati, uchafu, nia mbaya, tamaa mbaya na tamaa ya mali inayokuwa sawa vile kuabudu sanamu.
تلاش Wakolosayi 3:5
10
Wakolosayi 3:3
Kwa maana ninyi mumekufa na uzima wenu umefichwa pamoja na Kristo katika Mungu.
تلاش Wakolosayi 3:3
11
Wakolosayi 3:8
Lakini sasa mutupilie mbali mambo haya yote: kasirani, chuki, uovu, masingiziano na musiseme neno lolote baya.
تلاش Wakolosayi 3:8
12
Wakolosayi 3:9-10
Musiambiane uongo ninyi kwa ninyi, kwa maana mumeondoa utu wenu wa zamani pamoja na matendo yake na kuvaa utu mupya. Utu ule unaendelea kufanywa upya kila mara kufuatana na mufano wa Mungu anayekuwa muumba wake, kusudi mupate kumujua hakika.
تلاش Wakolosayi 3:9-10
13
Wakolosayi 3:19
Waume muwapende wake wenu nanyi musiwatendee kwa ukali.
تلاش Wakolosayi 3:19
14
Wakolosayi 3:20
Watoto muwatii wazazi wenu katika mambo yote, kwa maana jambo hili linamupendeza Bwana.
تلاش Wakolosayi 3:20
15
Wakolosayi 3:18
Wake muwatii waume wenu kama vile inavyostahili mbele ya Bwana.
تلاش Wakolosayi 3:18
صفحہ اول
بائبل
مطالعاتی منصوبہ
Videos