Injili Ulimwenguni - Sehemu 2Намуна

Kukataliwa kwa Yesu Nazareti
Kisha Yesu akarudi mpaka Galilaya, akiwa amejaa nguvu za Roho Mtakatifu, nazo habari zake zikaenea katika sehemu zote za nchi za kandokando.
Yesu akaenda Nazareti, hapo alipolelewa na siku ya Sabato alikwenda katika sinagogi kama ilivyokuwa desturi yake. Akasimama ili asome, naye akapewa kitabu cha nabii Isaya, akakifungua na kukuta mahali palipoandikwa:
“Roho wa Bwana yu juu yangu,
kwa sababu amenitia mafuta
kuwaletea maskini habari njema.
Amenituma kuwatangazia wafungwa
kufunguliwa kwao na vipofu kupata kuona tena,
kuwaweka huru wanaoonewa
na kutangaza mwaka wa Bwana uliokubalika.”
Kisha akakifunga kitabu, akamrudishia mtumishi na akaketi. Watu wote waliokuwamo katika sinagogi wakamkazia macho. Ndipo akaanza kwa kuwaambia, “Leo maandiko haya yametimia mkiwa mnasikia.”
Wote waliokuwako wakamsifu na kuyastaajabia maneno yake yaliyojaa neema, wakaulizana, “Je, huyu si mwana wa Yosefu?” Yesu akawaambia, “Bila shaka mtatumia mithali hii, ‘Tabibu, jiponye mwenyewe! Mambo yale tuliyosikia kwamba uliyafanya huko Kapernaumu, yafanye na hapa kwenye mji wako.’”
Yesu akasema, “Amin, nawaambia, hakuna nabii anayekubalika kwenye mji wake mwenyewe.
Lakini ukweli ni kwamba "palikuwa na wajane wengi katika Israeli wakati wa Eliya, mbingu zilipofungwa kwa miaka mitatu na miezi sita pakawa na njaa kuu katika nchi nzima.
Hata hivyo Eliya hakutumwa hata kwa mmoja wao, bali kwa mjane mmoja wa Sarepta katika nchi ya Sidoni.
"Pia palikuwa na wengi wenye ukoma katika Israeli katika siku za nabii Elisha, lakini hakuna hata mmoja wao aliyetakaswa, isipokuwa Naamani mtu wa Shamu.”
"Watu wote katika sinagogi waliposikia maneno haya, wakakasirika sana. Wakasimama, wakamtoa nje ya mji, wakamchukua hadi kwenye kilele cha mlima mahali ambapo mji huo ulikuwa umejengwa, ili wamtupe chini kutoka kwenye mtelemko mkali.
"Lakini yeye akapita papo hapo katikati ya huo umati wa watu akaenda zake.
Scripture
About this Plan

Mfuatano huu ni kusanyiko la hadithi kuhusu maisha Kristo itakayoshirikisha watazamaji wote ulimwenguni kwa kutumia mchanganyiko wa kuona na sauti. Maisha na mafundisho ya Yesu yalidhihirishwa katika kitabu hiki cha hadithi ambacho kinafuata masimulizi ya Agano Jipya yanayopatikana katika vitabu vya Injili vya Mathayo, Marko, Luka, na Yohana.
More
Нақшаҳои марбут ба мавзӯъ

Journey Through Jeremiah & Lamentations

Journey With Jesus: 3 Days of Spiritual Travel

The Way of St James (Camino De Santiago)

Prayer Altars: Embracing the Priestly Call to Prayer

Sickness Can Draw You and Others Closer to God, if You Let It – Here’s How

Live Like Devotional Series for Young People: Daniel

The Making of a Biblical Leader: 10 Principles for Leading Others Well

Journey Through Proverbs, Ecclesiastes & Job

How Stuff Works: Prayer
