Mwanzo UTANGULIZI

UTANGULIZI
Kitabu cha Mwanzo ndicho cha kwanza katika orodha ya vitabu vya Biblia. Jina Mwanzo linatokana na kitabu chenyewe (1:1) kwa maana ya asili na chanzo cha ulimwengu, mtu, dhambi, kifo na taifa la Israeli. Jambo la msingi ni Mungu na mtu katika uhusiano wao na pia mpango wa Mungu wa wokovu na uteule wa watu wa wake.
Mungu ndiye Muumba wa vitu vyote. Mungu alimwumba mtu, lakini mtu huyo alimwasi Muumba wake, na kwa uasi wake watu wote wakawa wenye dhambi. Matokeo ya dhambi yakawa kifo. Kwa kuwa tangu mwanzo Mungu aliahidi kuujalia uumbaji wake baraka zake. Ndipo hata mtu alipoasi, Mungu aliendelea kujifunua kwake, kunena na wateule wake, kuwapa wajibu na kuwabariki.
Yaliyomo:
1. Simulizi la awali kuhusu ulimwengu na mtu, Sura 1—11
(a) Kuumba ulimwengu (1—2)
(b) Uasi na kuanguka kwa mtu (3)
(c) Uasi unaongezeka (4—5)
(c) Nuhu na gharika (6—9)
(d) Mnara wa Babeli (10—11)
2. Historia ya awali ya Waisraeli, Sura 12—50
(a) Habari za Abrahamu na watoto wake (12—24)
(b) Habari za Yakobo (25—36)
(c) Habari za Yusufu (37—50)

선택된 구절:

Mwanzo UTANGULIZI: SRUV

하이라이트

공유

복사

None

모든 기기에 하이라이트를 저장하고 싶으신가요? 회원가입 혹은 로그인하세요

YouVersion은 여러분의 경험을 개인화하기 위해 쿠키를 사용합니다. 저희 웹사이트를 사용함으로써 여러분은 저희의 개인 정보 보호 정책에 설명된 쿠키 사용에 동의하게 됩니다