1
Matayo 7:7
BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002
SWC02
“Muombe, nanyi mutapewa; mutafute, nanyi mutapata; mupige hodi, nanyi mutafunguliwa mulango.
Bera saman
Njòttu Matayo 7:7
2
Matayo 7:8
Kwa maana kila mutu anayeomba, anapewa; naye anayetafuta, anapata, naye anayepiga hodi, anafunguliwa.
Njòttu Matayo 7:8
3
Matayo 7:24
“Basi kila mutu anayesikia hayo maneno yangu na kuyashika, anafananishwa na mutu mwenye akili aliyejenga nyumba yake juu ya jiwe.
Njòttu Matayo 7:24
4
Matayo 7:12
“Basi jambo lolote munalotaka wengine wawatendee, ninyi mulitende kwao vilevile, kwa maana kile ndicho kifungo cha Sheria ya Musa na mafundisho ya manabii.
Njòttu Matayo 7:12
5
Matayo 7:14
Lakini njia inayoongoza kufikia kwenye uzima ni yenye kusongamana na mulango unaoiingilia ni mwembamba, nao watu wanaoifuata ni wachache tu.
Njòttu Matayo 7:14
6
Matayo 7:13
“Muingie kwa kupitia mulango unaokuwa mwembamba. Kwa maana njia inayoongoza kufikia kwenye lufu ni kubwa, nao mulango unaoiingilia ni mupana, nao watu wanaoipitia ni wengi.
Njòttu Matayo 7:13
7
Matayo 7:11
Basi ikiwa ninyi munaokuwa waovu munajua kuwapa watoto wenu vitu vizuri, zaidi sana Baba yenu anayekuwa mbinguni atawapa wale wanaomwomba vitu vizuri zaidi.
Njòttu Matayo 7:11
8
Matayo 7:1-2
“Musiwahukumu wengine kusudi Mungu asiwahukumu ninyi vilevile. Kwa maana mutahukumiwa kufuatana na namna munavyowahukumu wengine, na kipimo kile munachowapimia wengine ndicho kitakachotumiwa kwenu vilevile.
Njòttu Matayo 7:1-2
9
Matayo 7:26
“Lakini kila mutu anayesikia maneno ninayotoka kusema bila kuyashika, anafananishwa na mutu mupumbafu aliyejenga nyumba yake juu ya udongo wenye kichanga.
Njòttu Matayo 7:26
10
Matayo 7:3-4
Namna gani unaona vumbi inayokuwa ndani ya jicho la ndugu yako, lakini haufikiri juu ya nguzo inayokuwa ndani ya jicho lako? Au namna gani unaweza kumwambia ndugu yako kwamba aache umwondoe vumbi inayokuwa ndani ya jicho lake, wakati ndani ya jicho lako mwenyewe mungali ile nguzo?
Njòttu Matayo 7:3-4
11
Matayo 7:15-16
“Mufanye angalisho na manabii wa uongo; kwa maana wanakuja kwenu wakionekana kwa inje kama vile kondoo, lakini ndani, wao ni kama imbwa wakali wa pori. Mutawatambua kwa matendo yao. Watu hawachumi matunda ya mizabibu au ya tini toka juu ya miti ya miiba.
Njòttu Matayo 7:15-16
12
Matayo 7:17
Na ni vile inavyokuwa: kila muti muzuri unazaa matunda mazuri, lakini kila muti mubaya unazaa matunda mabaya.
Njòttu Matayo 7:17
13
Matayo 7:18
Muti muzuri hauwezi kutoa matunda mabaya, wala muti mubaya hauwezi kutoa matunda mazuri.
Njòttu Matayo 7:18
14
Matayo 7:19
Kila muti usiozaa matunda mazuri unakatwa na kutupwa katika moto.
Njòttu Matayo 7:19