1
Matayo 4:4
BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002
SWC02
Yesu akamujibu: “Imeandikwa hivi katika Maandiko Matakatifu: ‘Mutu hawezi kuishi kwa mukate tu, lakini kwa njia ya kushika kila neno Mungu analosema.’ ”
Bera saman
Njòttu Matayo 4:4
2
Matayo 4:10
Lakini Yesu akamwambia: “Toka wewe, Shetani! Kwa maana imeandikwa: ‘Umwabudu Bwana Mungu wako na umutumikie yeye peke yake.’ ”
Njòttu Matayo 4:10
3
Matayo 4:7
Yesu akamujibu: “Imeandikwa hivi vilevile: ‘Usimujaribu Bwana Mungu wako.’ ”
Njòttu Matayo 4:7
4
Matayo 4:1-2
Kisha Roho Mutakatifu akamwongoza Yesu kwenda katika jangwa kusudi ajaribiwe na Shetani. Naye Yesu alipomaliza kufunga kula chakula kwa muda wa siku makumi ine, muchana na usiku, akasikia njaa.
Njòttu Matayo 4:1-2
5
Matayo 4:19-20
Yesu akawaambia: “Munifuate, nami nitawaweka kwa kazi ya kuopoa watu.” Mara moja wakaacha nyavu zao, na kumufuata.
Njòttu Matayo 4:19-20
6
Matayo 4:17
Tangia wakati huo Yesu akaanza kuhubiri, akisema: “Mugeuke toka zambi zenu, kwa maana Ufalme wa mbinguni umekaribia!”
Njòttu Matayo 4:17