Mimi nimemuchagua Bezaleli mwana wa Uri mwana wa Huri, wa kabila la Yuda na kumujaza Roho wangu. Nimemupatia ufahamu na akili, maarifa na ufundi, kusudi afanye kazi za ufundi na kufanya kazi za kufua zahabu, feza na shaba. Nimemupatia ujuzi wa kuchonga mawe ya kupamba, kuchonga mbao, na ujuzi wa kila aina ya ufundi.