Hesabu UTANGULIZI
UTANGULIZI
Jina la kitabu hiki: Hesabu, linatokana na hesabu mbili za watu ambazo zinatajwa katika kitabu chenyewe. Katika kitabu hiki tunaelezwa jinsi Musa alivyowahesabu Waisraeli mbele ya kuanza safari yao kutoka mulima Sinai, na tena nyuma katika inchi ya Moabu, upande wa mashariki wa Yordani. Kitabu chenyewe kinaeleza jinsi Waisraeli, nyuma ya kupokea maagizo yote ya Mungu kule Sinai, wakasafiri katika jangwa kuelekea inchi ya ahadi (1.1–10.10). Kwanza walifika Kadesi Barnea upande wa kusini wa inchi hiyo, lakini hawakuweza kuingia. Hivyo ikawapasa kukaa katika jangwa miaka makumi ine muda ambapo walijitayarisha na kwa mwisho wakaikamata inchi ya Moabu upande wa mashariki wa bahari ya Chumvi (10.11–21.35). Sura za mwisho za kitabu hiki zinasimulia juu ya matukio yaliyoelekea kutekwa kwa inchi ya Moabu; kutoka humo Waisraeli wakaingia katika inchi waliyoahidiwa (22.1–36.13).
Kitabu hiki ambacho kinafuata vile vya Mwanzo, Kutoka na Walawi kinatupatia picha ya Waisraeli katika hali yao kweli ya kibinadamu – wenye matumaini na mashaka, wenye nguvu na uzaifu. Kinaonyesha vilevile uaminifu wa Mungu katika kuwalinda watu wake.
Nke Ahọpụtara Ugbu A:
Hesabu UTANGULIZI: SWC02
Mee ka ọ bụrụ isi
Kesaa
Lee anya n'etiti ihe abụọ
Mapịa
Ịchọrọ ka echekwaara gị ihe ndị gasị ị mere ka ha pụta ìhè ná ngwaọrụ gị niile? Debanye aha gị ma ọ bụ mee mbanye
Bible in Swahili Congo © Bible Society of the Democratic Republic of Congo (DRC), 2002.