Akara Njirimara YouVersion
Akara Eji Eme Ọchịchọ

Hosea 13

13
1Waefuraimu waliposema, watu wote walitetemeka;
Waefuraimu walikuwa na uwezo mukubwa katika inchi ya Israeli,
lakini walianza kumwabudu mungu Bali, wakajiletea kifo.
2Waefuraimu wanaendelea kutenda zambi,
wanajitengenezea sanamu za feza yenye kuyeyushwa,
sanamu zinazotengenezwa kwa ufundi wao,
zote zikiwa kazi ya wafundi.
Wanasema: Muzitambikie!
Wanaume wanabusu sanamu ya mwana-ngombe!
3Basi, watatoweka kama ukungu wa asubui,
kama umande unaotoweka upesi;
kama makapi yanayopeperushwa kwenye nafasi ya kupepetea,
kama moshi unaotoka katika munara wa kutoshea moshi inje.
4Yawe anasema:
Lakini mimi ni Yawe, Mungu wenu,
niliyewatoa katika inchi ya Misri;
hakuna mungu mwingine lakini mimi,
wala hakuna anayeweza kuwaokoa.
5Ni mimi niliyewachunga mulipokuwa katika jangwa,
katika inchi iliyokuwa yenye kukauka.
6Lakini mulipokwisha kula na kushiba,
mulianza kuwa na kiburi, mpaka mukanisahau.
7Basi, nitakuwa kama simba kwenu ninyi wote;
nitawavizia kama chui katika njia.
8Nitawarukia kama dubu
aliyenyanganywa watoto wake.
Nitawararua vifua vyenu
na kuwakula palepale kama simba;
nitawararua vipandevipande kama nyama wa pori.
9Nitawaangamiza, enyi Waisraeli.
Nani ataweza kuwasaidia?
10Yuko wapi sasa mufalme wenu awaokoe?
Wako wapi wale wakubwa wenu wawalinde?
Ninyi ndio mulioomba:
Utupatie mufalme na wakubwa watutawale.
11Kwa hasira yangu mimi nikawapa mufalme,
kisha nikamwondoa kwa kasirani yangu.
12Uovu wa Efuraimu uko umeandikwa,
zambi yake imewekwa akiba.
13Maumivu kama ya kuzaa mutoto yanamufikia.
Lakini yeye ni mutoto mupumbafu;
wakati wa kuzaliwa unapofika
yeye anakataa kutoka ndani ya tumbo la mama!
14Inanipasa kuwakomboa hawa watu kutoka kuzimu;
sharti niwaokoe kutoka kifo!
Ewe kifo, mapigo yako ni wapi?
Ewe kuzimu, kuangamiza kwako ni wapi?
Mimi sitawaonea tena huruma!
15Hata kama Efuraimu atastawi kama nyasi,
mimi Yawe nitavumisha upepo mukali wa mashariki,
upepo utakaotokea kule katika jangwa,
nao utakausha visima vyake,
chemichemi zake zitakauka.
Vitu vyake vyote vya bei kali vitaharibiwa.

Nke Ahọpụtara Ugbu A:

Hosea 13: SWC02

Mee ka ọ bụrụ isi

Kesaa

Lee anya n'etiti ihe abụọ

Mapịa

None

Ịchọrọ ka echekwaara gị ihe ndị gasị ị mere ka ha pụta ìhè ná ngwaọrụ gị niile? Debanye aha gị ma ọ bụ mee mbanye