Hagai UTANGULIZI
UTANGULIZI
Tunavyoambiwa kwa mwanzo wa kitabu hiki, Hagai alihubiri kuanzia mwaka wa pili wa utawala wa Dario mufalme wa Persia, ni kusema katika mwaka wa 520 mbele ya Kristo, karibu miaka 20 nyuma ya Wayuda waliokuwa katika uhamisho kule Babeli kuruhusiwa na mufalme wa Persia kurudi kwao. Kundi la kwanza la Waisraeli lilirudi kwao kuanzia mwaka wa 538 mbele ya Kristo. Nyuma ya Wayuda kurudi kwao, walianza shuguli za kujenga upya hekalu lililoharibiwa na Wababeli katika mwaka wa 587. Lakini walikata tamaa; ndiyo maana nabii anawatia moyo waendelee. Anawatangazia kwamba, hekalu jipya litapendeza kuliko lile la kwanza (2.1-9) na kwamba ujenzi wake utamaliza hali ya uchafu na umasikini uliowapata watu wa Mungu (2.10-20). Hekalu inaitwa “Nyumba ya Yawe” katika kitabu hiki na katika vitabu vingi vingine.
Kwa maneno ya Hagai ya kuwapa watu moyo, aliwahimiza watu wa nyakati zake wakuwe na bidii na kuifanya kazi wakitazamia hali mupya ambayo Mungu amewatayarishia.
Nke Ahọpụtara Ugbu A:
Hagai UTANGULIZI: SWC02
Mee ka ọ bụrụ isi
Kesaa
Lee anya n'etiti ihe abụọ
Mapịa
Ịchọrọ ka echekwaara gị ihe ndị gasị ị mere ka ha pụta ìhè ná ngwaọrụ gị niile? Debanye aha gị ma ọ bụ mee mbanye
Bible in Swahili Congo © Bible Society of the Democratic Republic of Congo (DRC), 2002.