Akara Njirimara YouVersion
Akara Eji Eme Ọchịchọ

Amosi 4

4
1Musikilize neno hili,
enyi wanawake munaokuwa kama ngombe wa Basani
munaokuwa kule juu ya mulima wa Samaria.
Ninyi munaowaonea wamasikini,
munaowagandamiza wakosefu,
na kuwaambia waume zenu:#4.1 zenu: au: zao.
Mutuletee divai tukunywe!
Musikilize ujumbe huu:
2Bwana wetu Yawe Mutakatifu ameapa:
Siku zinakuja ambapo
watu watawakokota kwa ndoana kubwa,
kila mumoja wenu kama samaki kwenye ndoana.
3Mutakokotwa mpaka kwenye ukuta ulipobomolewa,
na kutupwa inje.
–Ni ujumbe wa Yawe.
Waisraeli hawajabadilika bado
4Enyi Waisraeli,
muende basi kule Beteli na kuniasi!
Muende Gilgali muongeze makosa yenu!
Mutoe sadaka zenu kila asubui
na zaka zenu kwa siku ya tatu.
5Mutoe sadaka ya shukrani ya mikate isiyotiwa chachu.
Mutangaze popote kwamba mumetoa kwa mapenzi;
maana ndivyo munavyopenda kufanya!
–Ni ujumbe wa Bwana wetu Yawe.–
6Mimi niliwanyima chochote cha kutafuna,
nikasababisha ukosefu wa chakula popote.
Hata hivyo hamukunirudilia.
–Ni ujumbe wa Yawe.–
7Tena niliwanyima mvua
miezi mitatu tu mbele ya mavuno.
Nilinyeshea mvua muji mumoja,
na muji mwingine nikaunyima.
Shamba moja lilipata mvua,
na lingine halikupata, likakauka.
8Watu wa miji miwili au mitatu wakakimbilia katika muji mwingine,
wapate maji, lakini hayakuwatoshelea.
Hata hivyo hamukunirudilia.
–Ni ujumbe wa Yawe.–
9Niliwapiga pigo la ukosefu wa maji na ukungu;
nikakausha bustani na mashamba yenu ya mizabibu;
nzige wakakula miti ya tini na mizeituni yenu.
Hata hivyo hamukunirudilia.
–Ni ujumbe wa Yawe.–
10Niliwaletea ugonjwa mukali
kama ule nilioupelekea Misri.
Niliwaua vijana wenu katika vita,
nikatwaa farasi wenu wa vita.
Maiti zilijaa katika kambi zenu,
harufu yake mbaya ikajaa katika pua zenu.
Hata hivyo hamukunirudilia.
–Ni ujumbe wa Yawe.–
11Niliwaangusha wamoja kati yenu kwa maangamizi
kama nilivyoangamiza Sodoma na Gomora.
Wale waliobaki kati yenu,
walikuwa kama kijiti kilichookolewa katika moto.
Hata hivyo hamukunirudilia.
–Ni ujumbe wa Yawe.–
12Kwa hiyo, enyi Waisraeli, nitawaazibu.
Na kwa sababu nitafanya jambo lile,
mujitayarishe kwa kutana na Mungu wenu!
13Mungu ndiye aliyeifanya milima,
na kuumba upepo;
ndiye anayemujulisha mwanadamu mawazo yake;
ndiye anayegeuza muchana kuwa usiku,
na kukanyaga vilele vya dunia.
Yawe wa majeshi ndilo jina lake!

Nke Ahọpụtara Ugbu A:

Amosi 4: SWC02

Mee ka ọ bụrụ isi

Kesaa

Lee anya n'etiti ihe abụọ

Mapịa

None

Ịchọrọ ka echekwaara gị ihe ndị gasị ị mere ka ha pụta ìhè ná ngwaọrụ gị niile? Debanye aha gị ma ọ bụ mee mbanye