1
Luka 8:15
BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002
SWC02
Nao udongo muzuri walimopanda mbegu, ni mufano wa watu wanaosikia neno la Mungu na kulishika kwa moyo mwema na kwa uhaki. Ndio wale wanaovumulia hata wanatoa matunda mazuri.
Lee anya n'etiti ihe abụọ
Nyochaa Luka 8:15
2
Luka 8:14
Na mbegu zilizoanguka katika miiba ni mufano wa wale wanaosikia, lakini masumbuko, utajiri na raha ya dunia vinawasonga hata wanashindwa kutoa matunda yanayokomaa.
Nyochaa Luka 8:14
3
Luka 8:13
Udongo wenye mawe pahali mbegu zilipoanguka ni mufano wa watu wanaosikia neno na kulipokea kwa furaha, lakini halizami ndani yao kama mizizi. Wanaliaminia kwa muda mufupi tu, nayo majaribu yanapowafikia, wanaliacha.
Nyochaa Luka 8:13
4
Luka 8:25
Halafu akawaambia wanafunzi wake: “Imani yenu iko wapi?” Nao wakaogopa na kushangaa, wakiulizana: “Huyu ni mutu gani? Anaamuru hata zoruba na ziwa, navyo vinamutii!”
Nyochaa Luka 8:25
5
Luka 8:12
Nafasi ile mbegu zilipoanguka pembeni ya njia ni mufano wa watu wanaosikia neno la Mungu. Lakini Shetani anakuja na kuondoa lile neno katika mioyo yao kusudi wasiamini na kuokolewa.
Nyochaa Luka 8:12
6
Luka 8:17
Na ni hivi hakuna chochote kinachofichwa kitakachokosa kuonekana wazi, wala hakuna siri itakayokosa kufunuliwa waziwazi.
Nyochaa Luka 8:17
7
Luka 8:47-48
Yule mwanamuke alipoona kwamba ametambulikana, akakuja akitetemeka kwa woga na kujitupa mbele ya Yesu. Na pale mbele ya watu wote, akaeleza sababu gani alimugusa na namna alivyoponyeshwa mara moja. Na Yesu akamwambia: “Binti yangu, imani yako imekuponyesha. Ujiendee na amani.”
Nyochaa Luka 8:47-48
8
Luka 8:24
Basi wanafunzi wake wakamujongelea, wakamwamusha wakisema: “Bwana, Bwana, tunakufa!” Yesu alipoamuka, akakaripia zoruba, nayo ikakoma na maji yakatulia.
Nyochaa Luka 8:24