1
Mathayo 7:7
Biblia Habari Njema
BHN
“Ombeni, nanyi mtapewa; tafuteni, nanyi mtapata; bisheni mlango, nanyi mtafunguliwa.
Sammenlign
Udforsk Mathayo 7:7
2
Mathayo 7:8
Maana, yeyote aombaye hupewa, atafutaye hupata, na abishaye mlango hufunguliwa.
Udforsk Mathayo 7:8
3
Mathayo 7:24
“Kwa hiyo, kila mtu anayeyasikia maneno yangu na kuyazingatia, anafanana na mtu mwenye busara, aliyejenga nyumba yake juu ya mwamba.
Udforsk Mathayo 7:24
4
Mathayo 7:12
“Yote mnayotaka watu wawatendee nyinyi, watendeeni wao vivyo hivyo. Hii ndiyo maana ya sheria ya Mose na mafundisho ya manabii.
Udforsk Mathayo 7:12
5
Mathayo 7:14
Lakini njia inayoongoza kwenye uhai ni nyembamba, na mlango wa kuingilia humo ni mwembamba; ni watu wachache tu wanaoweza kuigundua njia hiyo.
Udforsk Mathayo 7:14
6
Mathayo 7:13
“Ingieni kwa kupitia mlango mwembamba. Kwa maana njia inayoongoza kwenye maangamizi ni pana, na mlango wa kuingilia humo ni mpana; waendao njia hiyo ni wengi.
Udforsk Mathayo 7:13
7
Mathayo 7:11
Kama basi nyinyi, ingawa ni waovu, mwajua kuwapa watoto wenu vitu vizuri, hakika Baba yenu wa mbinguni atafanya zaidi: Atawapa mema wale wanaomwomba.
Udforsk Mathayo 7:11
8
Mathayo 7:1-2
“Msiwahukumu wengine, msije nanyi mkahukumiwa na Mungu; kwa maana jinsi mnavyowahukumu wengine, ndivyo nanyi mtakavyohukumiwa; na kipimo kilekile mnachotumia kwa wengine ndicho Mungu atakachotumia kwenu.
Udforsk Mathayo 7:1-2
9
Mathayo 7:26
“Lakini yeyote anayesikia maneno yangu haya bila kuyazingatia, anafanana na mtu mpumbavu aliyejenga nyumba yake juu ya mchanga.
Udforsk Mathayo 7:26
10
Mathayo 7:3-4
Kwa nini wakiona kibanzi kilicho jichoni mwa ndugu yako, na papo hapo huioni boriti iliyoko jichoni mwako? Au, wawezaje kumwambia ndugu yako, ‘Ndugu, ngoja nikuondoe kibanzi jichoni mwako,’ wakati wewe mwenyewe unayo boriti jichoni mwako?
Udforsk Mathayo 7:3-4
11
Mathayo 7:15-16
“Jihadharini na manabii wa uongo. Wao huja kwenu wakionekana kama kondoo kwa nje, lakini kwa ndani ni mbwamwitu wakali. Mtawatambua kwa matendo yao. Je, watu huchuma zabibu katika miti ya miiba, au tini katika mbigili? La!
Udforsk Mathayo 7:15-16
12
Mathayo 7:17
Basi, mti mzuri huzaa matunda mazuri, na mti mbaya huzaa matunda mabaya.
Udforsk Mathayo 7:17
13
Mathayo 7:18
Mti mzuri hauwezi kuzaa matunda mabaya, wala mti mbaya hauwezi kuzaa matunda mazuri.
Udforsk Mathayo 7:18
14
Mathayo 7:19
Kila mti usiozaa matunda mazuri utakatwa na kutupwa motoni.
Udforsk Mathayo 7:19